Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Ziara ya Rais Magufuli yang’oa kigogo Ruvuma
Habari Mchanganyiko

Ziara ya Rais Magufuli yang’oa kigogo Ruvuma

Spread the love

RAIS John Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma, Dk. Oscar Mbyuzi. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Taarifa ya utenguzi huo imetolewa leo tarehe 9 Aprili 2019 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa.

Taarifa ya Msigwa inaeleza kuwa, Rais Magufuli amemteua Jimson Mhagama kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa.

“Uteuzi wa Bw. Mhagama unaanza mara moja leo tarehe 9 Aprili 2019,” inaeleza sehemu ya taarifa ya Msigwa.

Hata hivyo, taarifa ya Msigwa haikueleza sababu za utenguzi wa Mbyuzi.

Hatua hiyo ya Rais Magufuli imekuja siku moja baada ya kiongozi huyo mkuu wa nchi kumaliza ziara yake ya kikazi ya siku sita mkoani Ruvuma.

Katika ziara yake hiyo mkoani Ruvuma iliyoanza tarehe 4 hadi 9 Aprili mwaka huu, Rais Magufuli alizindua miradi mbalimbali ikiwemo barabara ya Tunduru-Matemanga-Namtumbo, pamoja na ujenzi wa Chuo cha Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) wilayani Namtumbo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

TMA yaagizwa kutangaza mafanikio yao kikanda, kimataifa

Spread the love  KATIBU Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara ameiagiza...

Habari Mchanganyiko

NMB yasaidia waathirika wa mafuriko, maporomoko Hanang

Spread the loveWaathirika wa maporomoko ya tope Wilayani Hanang, mkoani Manyara, waliopoteza...

Habari Mchanganyiko

TPF-NET Arusha yaonya jamii ya wafugaji zinazoendeleza ukatili wa watoto na wanawake

Spread the love  MTANDAO wa Polisi wanawake wa Arusha kuelekea siku 12...

Habari Mchanganyiko

Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Greyhorse zasaini mkataba wa bil.7.4

Spread the loveTAASISI ya Mwalimu Nyerere (MNF) imesaini mkataba wa miaka 10...

error: Content is protected !!