Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe apigiwa kura za ndio Hai, wawili wamkataa
Habari za Siasa

Mbowe apigiwa kura za ndio Hai, wawili wamkataa

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa
Spread the love

FREEMAN Mbowe, Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Upinzani Tanzania Chadema ameshinda kura za maoni za kuwani Ubunge wa Hai Mkoa wa Kilimanjaro katika Uchaguzi Mkuu wa tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Hai … (endelea).

Mbowe amepigiwa kura za maoni jana Jumamosi tarehe 25 Julai 2020 na wajumbe wa mkutano mkuu wa Jimbo hilo uliofanyika ukumbi wa KKKT jimboni humo akiwa mgombea pekee wa nafasi hiyo.

Akitangaza matokeo hayo, msimamizi wa uchaguzi huo, Michael Kilawaila amesema, Mbowe alipigiwa kura 203 za ndio na mbili za hapana.

Aidha katika uchaguzi huo, aliyekuwa mwenyekiti wa halmashauri ya Hai, Helga Mchomvu alipata kura 33 kati ya kura 66 zilizopigwa na wajumbe za nafasi ya ubunge wa viti maalum, wa pili ambaye ni Doris Mushi akipata kura 28 na watatu ni Irene Lema aliyepata kura 4.

Katika mkutano huo, Mbowe aliwashukuru wajumbe wote kwa kumuanini na kumpa nafasi hiyo tena ya kugombea ubunge jimbo la Hai akiwaahidi kuwavusha.

”Nawashukuru wote mlioonyesha imani na mimi kwa kufanya kampeni nzuri na ya kistaarabu na ya kijasiri sana, Mungu awabariki ninyi nyote. Tuendelee kuipigania haki ya kila mmoja wetu,” alisema Mbowe

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!