Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Muuza matikiti ambwaga diwani aliyeongoza miaka 20
Habari Mchanganyiko

Muuza matikiti ambwaga diwani aliyeongoza miaka 20

Paul Kabugwe, kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katikati
Spread the love

PAUL Kabugwe, kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ameacha historia kwa kumbwaga katika kura za maoni Ibrahimu Kalunga, aliyekuwa diwani wa Kata ya Nyakaliro, Sengerema mkaoni Mwanza kwa miaka 20. Anaripoti Mwandishi Wetu, Sengerema … (endelea).

Kabugwe ni ni mjasilimali anayejishughulisha na uuzaji wa matikiti maji Kata ya Nyakaliro Wilayani Sengerema

Akitangaza matokeo hayo, msimamizi wa uchaguzi huo Masumbuko Bihemo amesema, Kabugwe amepata kura 87 ambapo Kalunga aliyekuwa akitetea nafasi yake akipata kura 40.

“Wagombea katika nafasi hiyo walikuwa wanane, wapiga kura walikuwa 138 na kura zilizoharibika zilikuwa nane. Wagembea wengine mmoja kapata kura tatu na mwingine 0,” ameeleza Bihemo.

Wilaya ya Sengerema ina juma ya Kata 47, hata hivyo ni kata 16 tu ndiyo waliokuwa madiwani wake wamefanikiwa kutetea nafasi zao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

error: Content is protected !!