Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbatia ‘amwita’ Mbowe, Zitto mezani
Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ‘amwita’ Mbowe, Zitto mezani

James Mbatia, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi
Spread the love

FREEMAN Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Zitto Kabwe, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, ‘wamealikwa’ kwenye meza ya mazungumzo na James Mbatia, Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Bila kuwataja majina, Mbatia amesema, anawaalika vyama vya siasa vya upinzani kuzungumzia ushirikiano kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktba 2020.

“Sina tatizo la kuwa na maridhiano na vyama vingine,” amesema Mbatia leo Alhamisi tarehe 4 Juni 2020, jijini Dodoma alipozungumza na waandishi wa habari.

“Kinachonipa shida na taabu, ni kuona baadhi ya wanasiasa wakitukana kwenye mitandao juu ya watu wanaohama chama kimoja kuingia chama kingine.”

Mbatia ametoa kauli hiyo ikiwa ni siku moja baada ya John Mnyika, Katibu Mkuu wa Chadema kufungua milango ya ushirikiano na vyama vingine vya siasa nchini.

“Tunafungua mlango wa majadiliano na vyama ambavyo vinadhamira ya kweli ya kushirikiana kuiondoa CCM madarakani,” alisema Mnyika.

Chadema ndio chama kikuu cha upinzani nchini. Kwenye uchaguzi huo, zaidi ya vyama 15 vya upinzani vikiwemo CUF, ADC, UDP, UPDP, TADEA, TLP, UDP, CHAUSTA, PPT-MAENDELEO, SAU, ADC, CHAUMMA, AFP, CCK, NCCR-MAGEUZI, CHADEMA na ACT-WAZALENDO vinatarajiwa kushiriki.

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema (kushoto) akiwa na Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe

Akizungumzi msimamo wa chama hicho kuelekea uchaguzi mkuu, mwenyekiti huyo wa NCCR-Mageuzi na Mbunge wa Vunjo, Kilimanjaro amesema, kwenye siasa kinachosimama ni kushindana kwa hoja na si vinginevyo.

Mbatia amekumbusha kwamba, kupitia chama hicho Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) uliundwa na kwamba, chama hicho kinaamini kwenye ushirikiano na umoja.

“NCCR-Mageuzi ni kati ya vyama vya siasa ambavyo vinaamini kwenye ushirikiano. Hata Ukawa ni zao la NCCR. Naisitiza chama chetu kinaamini ushirikiano naumoja,” amesema.

Mwenyekiti huyo amesema, chama chake kinahamasisha vijana na akina mama kugombea nafasi mbalimbali za uchaguzi ndani ya chama hicho.

Ukawa ulianzishwa mwaka 2014 wakati wa Bunge Maalum la Katiba na ukaendelea katika uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 25 Oktoba 2020.

Katika uchaguzi huo, Ukawa uliokuwa ukujumuisha vyama vya CUF, NLD, CHADEMA na NCCR-MAGEUZI vilishirikiana kwa kusimamisha wagombea mmoja katika kata, jimbo na urais.

Hata hivyo, baadhi ya kata na majimbo, haukufanikiwa kwani walisimama wagombea zaidi ya mmoja kutoka Ukawa

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!