Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba
Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the love

Msemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Damas Ndumbaro kuhusu ukaguzi wa pasipoti kwa mashabiki watakaovaa jezi za timu za Mamemodi Sundown na Al Ahly kuwa ulikuwa ni utani. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Dk. Ndumbaro alisema mashabiki hao ambao wataingia katika Uwanja wa Benjamini Mkapa kushangilia kwenye michezo ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika itakayohusisha Simba na Yanga kati ya timu hizo za Afrika Kusini na Misri, watatakiwa kuonesha pasipoti za uraia wa nchi hizo.

Matinyi ametoa ufafanuzi huo leo Jumapili wakati akizungumza na wahariri na waandishi wa habari kutoja vyombo mbalimbali leo Jumapili kuhudu miaka miatu ya Serikali ya Awamu ya Sita ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Amesema “Katika lugha za michezo utani ni kitu cha kawaida, mnapozungumza 80% ni utani na 20 ndio ukweli, mkizungumza habari za Simba na Yanga ukang’ang’ana kitu kama kilivyoandikwa utafika hatua utawachosha watu.

“Hizo ni timu ambazo zinapenda utani, zinapokea ujumbe katika lugha rahisi, si kweli kuwa Waziri alimaanisha kutakuwa na ukaguzi wa Passport, anayehusika na ukaguzi halali ni Idara ya Uhamiaji ambayo hakuitaja alipozungumza,” amesema.

Matinyi ameongeza kuwa “Watu wamekomaa na utani hadi Mamelodi wamesikia, wameingia uoga hadi TFF wameamua kuandika barua kuwaeleza suala hilo halipo.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!