Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mashahidi 9 kutumika kesi ya kimtandao inayomkabili Mwandishi wa Habari
Habari Mchanganyiko

Mashahidi 9 kutumika kesi ya kimtandao inayomkabili Mwandishi wa Habari

Spread the love

MASHAHIDI tisa na vielelezo kumi vitatumika  katika kesi namba 407 ya 2022 ya kimtandao katika kundi la whassap inayokambili  mwandishi wa habari za afya na uchunguzi  wa gazeti la Raia Mwema Mary Victor na wenzake wawili Asha Mahita na Rogers Simeo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akiahirisha kesi hiyo mapema wiki hii, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala Glory Nkwera alisema  mashahidi tisa wataitwa kutoa ushahidi wao pamoja na vielelezo kumi vitatumika kama ushahidi mahakamani hapo Januari 17 kesi hiyo itakapoanza kusikilizwa.

Katika kesi hiyo  Maria Victor anatuhumiwa na makosa matatu likiwemo la kutumia laini ya simu ambayo imesajiliwa kwa jina la mtu mwingine(Asha Mahita), na pia kutuma taarifa ya uongo kuhusu maradhi ya Covid katika kundi la waandishi la whassap.

Naye Asha Mahita na Rogers wanatuhumiwa kwa pamoja  kushindwa kutoa taarifa kwa Mamlaka ya Mawasiliano(TCRA)mabadiliko ya umiliki wa laini hiyo ya simu yenye namba 0715166210.

 Katika kesi hiyo Mary na wenzake wanawakilishwa  na wakili kutoka Taasisi ya Sibaba Alex Masaba na wakili kutoka Shirika lisilo la Kiserikali la Tanzania Anti Human Traffic and legal Initiatives Frank Mposso.

Akizungumza na Raia Mwema mahakamani hapo mapema hivi karibuni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la TATILI Godrey Mpandikizi alisema: “Tumeamua  kuongeza nguvu ya kisheria tukishirikiana na wakili mwenzetu Alex Masaba kuhakikisha  haki inatendeka;

“Mwandishi wa habari anapofanya wajibu wake kihabari hatakiwi kupata vitisho au misukosuko ya aina yoyote  ile kwa sababu  anatimiza moja ya jukumu lake, taasisi yetu kama mdau wa waandishi wa habari  ina jukumu kubwa kumsaidia mwandishi wa habari au chombo chochote  cha habari.

“Ndio maana taasisi yetu inatoa mchango wa hali na mali kisheria kuhakikisha mwandishi anakuwa salama na kuendelea kutimiza majukumu yake kama kawaida.

Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa tena Januari 17 mwakani(2023) na washitakiwa wote wamekana mashitaka na wapo nje kwa dhamana huku simu za baadhi ya washtakiwa, vitambulisho vyao ikiwemo simu mmoja wa wakurugenzi Mbaraka Islam  zikiendelea kushikiliwa katika kituo cha polisi kati(central).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

error: Content is protected !!