Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Makontena ya Makonda kupigwa mnada J’mosi
Habari za Siasa

Makontena ya Makonda kupigwa mnada J’mosi

Spread the love

BAADA ya mnada wa kwanza wa makontena 20 yenye samani yaliyoingizwa na Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kukwama, Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imepanga kufanya mnada wa pili Jumamosi ya Septemba mosi, 2018. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

TRA imetaarifu kuwa, imedhamiri kurudia mnada huo wa makontena yenye samani za ofisi ikiwemo meza na viti, ambayo yamekwama katika bandari kavu ya Dar es Salaam kutokana na kudaiwa kodi ya kaisi cha Sh. 1.2 bilioni.

Mamlaka hiyo imetoa wito kwa wananchi kujitokeza katika mnada huo kununua samani hizo kwa kufuata taratibu na sheria za minada.

Aidha, TRA imewatoa hofu wananchi kuhusu kauli iliyotolewa na Makonda ya kwamba atakaye nunua makontena hayo atalaaniwa na Mungu.

Baada ya mnada wa kwanza uliofanyika tarehe 25 Agosti, 2018 kukwama kutokana na wateja kushindwa kufika bei elekezi, Makonda alitoa kauli akisema kuwa, mtu atakayenunua makontena hayo atapata laana kwa kuwa, makontena hayo yenye samani yaliingizwa nchini kwa ajili ya kuwasaidia waalimu wa mkoa wa Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!