Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Majaliwa atoa maagizo kwa wenyeviti vijiji, vitongoji
Habari Mchanganyiko

Majaliwa atoa maagizo kwa wenyeviti vijiji, vitongoji

Spread the love

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amewataka wenyeviti wa vijiji na vitongoji kutekeleza majukumu yao kwa uwazi, ikiwemo kuitisha mikutano ya wananchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Lindi…(endelea).

Waziri Mkuu ametoa maagizo hayo leo Alhamisi, tarehe 14 Aprili 2022, akifungua mafunzo ya utawala bora ya viongozi ngazi ya kata na vijiji, wilayani Ruangwa Mkoa wa Lindi.

“Niemsikia kuwa ipo mada ya utawala bora na hasa uwazi na uwajibikaji. Jambo hili ni muhimu sana, wewe kama kiongozi kila unachokifanya hakikisha kinakuwa wazi. Hakuna haja ya kuficha, hili jambo lina maslahi kwa umma kwa hiyo suala la uwazi na uwajibikaji ni muhimu sana,” amesema Majaliwa.

Majaliwa amewaagiza viongozi hao wa vijiji, kuwashirikisha wananchi katika shughuli mbalimbali, ikiwemo ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao.

“Nendeni mkawe wawazi, uwazi ni moja ya msingi mkubwa wa utawala bora, niwatake viongozi wote kuhakikisha wananchi wanapata taarifa za kila siku za shughuli za kijiji chenu. Nendeni mkaitishe vikao vya vijiji,” amesema Majaliwa.

Katika hatua nyingine, Kiongozi huyo amewataka wenyeviti wa vijiji na vitongoji, wakahamasishe mbio za mwenge zinazoendelea nchini.

“Nendeni mkahamasishe mbio za mwenge kama moja ya alama za nchi yetu, mwenge ni alama ya taifa, falsafa yake kuwaunganisha Watanzania kuwa pamoja. Mwenge una kazi kubwa kuhamasisha maendeleo kwenye nchi hii na lengo nchi iwe kwenye maendeleo tupae ikiwezekana tuzidi nchi zote,” amesema Waziri Majaliwa.

Aidha, Waziri Majaliwa amewataka waheshimu mipaka ya madaraka yao.

“Inawezekana mmekuja hapa wenyeviti wa vijiji na vitongoji, wote ni wenyeviti lakini mtambue mipaka yenu, isije tukasikia kuna migogoro ya mwenyekiti wa kijiji.

“Hakuna sababu ya kugombana na kama mamlaka zinafanana mnagombania juu ya jambo linalohusisha pande mbili, hakuna haja ya kutunishia misuli, tuna sheria na kanuni lazima zizingatiwe,” amesema Waziri Majaliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!