Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari Majaji wamkalia kooni Rostam, aomba radhi
HabariTangulizi

Majaji wamkalia kooni Rostam, aomba radhi

Rostam Azizi
Spread the love

 

MFANYABIASHARA maarufu nchini Tanzania, Rostam Aziz, ameomba radhi kufuatia kauli yake iliyodai kuwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, haiko huru kutokana na baadhi ya mahakimu wake kuendesha kesi kwa kufuatia maelekezo kutoka serikalini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari jini Dar es Salaam, leo Jumanne, Rostam amedai kauli hiyo aliitoa kwa kuteleza.

Mfanyabiashara hiyo ameomba radhi baada ya Chama cha Majaji na Mahakimu Tanzania (JMAT), kumtaka aombe radhi au athibitishe tuhuma zake kama ni kweli.

“Nimesoma taarifa ya chama cha majaji na Mahakimu, ningependa kuwahakikishia Umma kwamba wakati nazungumzia kuhusu uwekezaji wangu halikuwa kusudi langu kudharau mahakama zetu. Nilimaanisha mahakama zetu ziendane na kiwango cha kimataifa kuheshimu uwekezaji. Hivyo niliteleza,” amesema Rostam.

JMAT ilitoa wito kwa Rostam aombe radhi, Leo tarehe 4 Julai 2023, kupitia tangazo lake ililitoa kwenye gazeti la The Citizens.

Kupitia tangazo hilo, JMAT imesema halijawahi kupokea tuhuma au lalamiko lolote kutoka kwa mtu kuonyesha afisa wa Mahakama kupigiwa simu na kuelekezwa namna ya kutoa maamuzi katika Mahakama hiyo.

Tangazo hilo limesema, Mahakama ni chombo pekee cha utoaji haki nchini kwa mujibu wa Katiba na huendesha shughuli zake kwa uhuru bila kuingiliwa na mtu au chombo chochote.

JMAT kimesema kauli iliyotolewa na Rostam inahatarisha uhusiano na ushirikiano katika mihimili mitatu ya dola ndani ya nchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

error: Content is protected !!