Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mahakama yawaachia Bwege na wenzake, Polisi yawang’ang’ania
Habari za SiasaTangulizi

Mahakama yawaachia Bwege na wenzake, Polisi yawang’ang’ania

Spread the love

MAHAKAMA ya Mkoa wa Lindi imewaachia kwa dhamana viongozi waandamizi wa Chama cha Wananchi (CUF), waliokamatwa juzi kwenye kampeni za udiwani Kata ya Kivinje, Kilwa huku Jeshi la Polisi likiendelea kuwashikilia kwa kilichotajwa kuwa wamekosea usajili wa majina yao. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Viongozi hao waliokamatwa tangu juzi jioni tarehe 20 Novemba mwaka huu kwa tuhumiwa ya kutamka maneno ya uchochezi ni pamoja na Suleiman Bungara ‘Bwege,’mbunge wa chama hicho katika jimbo la Kilwa Kusini.

Wengine, ni Naibu Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa chama hicho, Mbarala Maharagande, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kilwa, Abuu Mjaka na mjumbe wa Kamati Tendaji.

Kwenye mahakama hiyo watuhumiwa hao wamesomewa mashtaka matano yakiwamo ya kutamka meneno ya uchochezi.

Shitaka la kwanza ni la uchochezi linalowakabili watuhumiwa wote watatu kwa kutamka maneno yanayoweza kuhatarisha amani kwenye mkutano wa kampeni za udiwani kwenye Kata ya Kivinje.

La pili ni linamkabili Bungara Mbunge wa Kilwa Kusini la kutamka maneno ya kutishia amani, shitaka la tatu halikusomwa kutokana na mshtakiwa wa kosa hilo Hamidu Bobali Mbunge wa Mchinga hakuwepo mahakamani hapo.

Shitaka la nne linamkabili Maharagande, kwa kutamka maneno ya vitisho kwenye hadhara ambapo shtaka la tano linamkabili Mjaka kutuhumiwa kutoa maneno ya matusi kwa wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambapo anadaiwa kusema “ukimuona mwana CCM ujue huyo mshipa wake wa akili umeungana na mshipa wa mavi.”

Shauri hilo limeahirishwa mpaka tarehe 3 Desemba, mwaka huu na kwamba watuhimiwa wameachiwa kwa dhamana ya mahakama.

Baada ya kukamilishwa kwa taratibu hizo jeshi la polisi liliendelea kuwashikilia viongozi hao kwa kilichodaiwa kuwa wamekosea kuyasajili majina yao.

Inadaiwa kuwa jeshi hilo limeshindwa kufanya marekebisho hayo leo kwa kile kilichoelezwa kuwa muda wa kazi umeisha hivyo watuhumiwa wataendelea kushikiliwa mpaka kesho asaubuhi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Afya ya akili yatajwa chanzo kuvunjika ndoa

Spread the loveCHANGAMOTO ya afya ya akili, imetajwa kuwa chanzo cha migogoro...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!