Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli awapa ulaji Prof. Kabudi, Bulembo
Habari za Siasa

Magufuli awapa ulaji Prof. Kabudi, Bulembo

Rais John Magufuli (kulia) akizungumza na Abdallah Bulembo, Mwenyekiti wa Umoja wa Wazazi wa CCM, Ikulu jijini Dar es Salaam
Spread the love

RAIS John Magufuli ametangaza kumteua Profesa Palamagamba Kabudi, na Abdallah Bulembo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi ya Chama Cha Mapinduzi kuwa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, anaandika Charles William.

Prof. Kabudi ni mhadhiri katika Kitivo cha Sheria, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Katibu wa Baraza la chuo hicho. Anakumbukwa na wengi kutokana na umahiri wa kujenga hoja aliouonesha wakati akiwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, maarufu kama tume ya Jaji Warioba.

Taarifa iliyotolewa leo na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu imesema kuwa, wabunge hao wawili wanatarajia kuapishwa hivi karibuni kulingana na utaratibu wa Bunge.

Uteuzi wa Prof. Kabudi na Bulembo umezua mijadala mbalimbali huku minong’ono ya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri ikianza kusikika, hasa uteuzi wa Prof. Kabudi ukidhaniwa kwamba huenda ikawa ni hatua moja mbele kabla ya kumteua kuwa waziri.

Bulembo anakumbukwa zaidi kwa kazi kubwa ya kusimamia kampeni za Rais Magufuli katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 ambapo ndiye aliyekuwa mkuu wa msafara wa kampeni hizo, akizunguka karibu nchi nzima pamoja na aliyekuwa mgombea wa CCM.

Bulembo alishatangaza kutomuendelea na siasa za ndani za CCM kwa maana ya kugombea katika uchaguzi mkuu wa chama hicho utakaofanyika mwaka huu na hivyo uteuzi wa Rais Magufuli unaashiria kuendelea kumbakiza mwanasiasa huyo katika medani ya siasa kupitia Bunge.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!