MWENYEKITI wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu Semistocles Kaijage amemteua Yeremia Maganja wa NCCR-Mageuzi kuwa mgombea urais wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu wa 28 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Pia, Jaji Kaijage amemteua Haji Ambar Khamisi kuwa mgombea mwenza. Maganja amekuwa mgombea wa sita kuteuliwa na NEC kugombea katika uchaguzi huo.
Jumla ya wagombea 17 walichukua fomu za uteuzi na mpaka sasa vimerudisha sita na wagombea wote wa vyama hivyo wameteuliwa na NEC.
Wengine waliokwisha teuliwa ni; John Pombe Magufuli wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Leopard Mahona (NRA), John Shibuda (Ada Tadea), Mutamwega Mgaiwa wa (SAU) na Cecilia Mwanga wa Demokrasia Makini.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI TV na mitandao yetu ya kijamii kwa taarifa na habari mbalimbali
Leave a comment