Saturday , 2 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Maganja wa NCCR-Mageuzi ateuliwa kugombea urais Tanzania
Habari za Siasa

Maganja wa NCCR-Mageuzi ateuliwa kugombea urais Tanzania

Yeremia Maganja wa NCCR-Mageuzi kuwa mgombea urais wa Tanzania
Spread the love

MWENYEKITI wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu Semistocles Kaijage amemteua Yeremia Maganja wa NCCR-Mageuzi kuwa mgombea urais wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu wa 28 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Pia, Jaji Kaijage amemteua Haji Ambar Khamisi kuwa mgombea mwenza. Maganja amekuwa mgombea wa sita kuteuliwa na NEC kugombea katika uchaguzi huo.

Jumla ya wagombea 17 walichukua fomu za uteuzi na mpaka sasa vimerudisha sita na wagombea wote wa vyama hivyo wameteuliwa na NEC.

Wengine waliokwisha teuliwa ni; John Pombe Magufuli wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Leopard Mahona (NRA), John Shibuda (Ada Tadea),  Mutamwega Mgaiwa wa (SAU) na Cecilia Mwanga wa Demokrasia Makini.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI TV na mitandao yetu ya kijamii kwa taarifa na habari mbalimbali

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia kuzindua programu ya nishati safi ya kupikia kwa wanawake Afrika

Spread the loveRais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua programu ya...

Habari za Siasa

AG aiagiza kamati ya maadili kuwashughulikia mawakili wanaokiuka maadili

Spread the loveMWANASHERIA Mkuu wa Serikali (AG), Dk. Eliezer Feleshi, ameagiza Kamati...

Habari za Siasa

Jaji avunja ukimya sakata la Mpoki kusimamishwa uwakili

Spread the loveJAJI Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma, amekitaka Chama cha...

Habari za Siasa

Sheikh Ponda ataka mwarobaini changamoto uchaguzi 2020

Spread the loveKATIBU Mkuu wa Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa...

error: Content is protected !!