Monday , 13 May 2024
Home Kitengo Biashara Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi
BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the love

Zaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS inayomiliki maabara ya upimaji wa sampuli za madini kwa kiwango cha kimataifa mkoani Geita.  Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Hayo yamebainishwa jana tarehe 27 2023 na Mkurugenzi  Mtendaji wa kampuni ya MSALABS, Mugisha Lwekoramu wakati wa ufunguzi wa maabara hiyo.

Akizungumzia kuhusu teknolojia inayotumika katika maabara hiyo Lweramu amesema inatumia teknolojia ya kisasa ya upimaji wa sampuli kwa njia ya mionzi yaani (PhotoAssay) ambayo ni rafiki kwa utunzaji mazingira kwasababu haitumii kemikali au moto katika upimaji sampuli.

Lwekoramu amesema  maabara hiyo ni sehemu ya mapinduzi ya teknolojia kwa sababu inamwezesha mdau kupata majibu ya sampuli ndani ya saa mbili ukilinganishwa na teknolojia ya zamani ya kutumia moto na kemikali.

Kwa upande wake Waziri wa Madini, Anthony Mavunde amempongeza Mkurugenzi huyo kwa kufanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya madini na kumtaka kuendelea kufungua matawi mengine nchini.

Aidha, amewapongeza pia kwa kuweza kuajiri watanzania kwa asilimia 99.8 akiamini kuwa wafanyakazi hao wataendelea kujifunza utumiaji wa teknolojia hiyo na kutoa ujuzi huo kwa watanzania wengine.

Mavunde ameahidi kuwa Serikali itaendelea kuwatengenezea mazingira rafiki ya uwekezaji na kutoa ushirikiano kwa jinsi itakavyohitajika katika mnyororo mzima wa sekta ya madini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Biashara

Meridianbet yatoa msaada Kigamboni siku ya Mama Duniani

Spread the loveMABIBGWA wa michezo ya kubashiri kampuni yaMeridianbet imefika kigamboni leo siku...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Biteko: Serikali itaendelea kushirikiana na Red Cross

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Dk.Mpango aagiza trafki kuvaa makoti ya kamera kudhibiti rushwa

Spread the loveMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk....

BiasharaHabari Mchanganyiko

PPAA yajipanga kuwanoa wazabuni namna kuwasilisha rufaa kieletroniki

Spread the loveIli kukabiliana na mageuzi yaliyofanyika katika Sheria mpya ya Ununuzi...

error: Content is protected !!