Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu: …yaani hata sijui
Habari za Siasa

Lissu: …yaani hata sijui

Tundu Lissu, Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chadema
Spread the love

TUNDU Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amesema watu wanaofurika kwenye mikutano yake ya kampeni za urais, hajui kama ni wapiga kura. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza…(endelea).

Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari jijini Mwanza jana Jumamosi tarehe 26 Septemba 2020, Lissu alitoa kauli hiyo alipoulizwa na mwandishi siri ya mafanikio ya kampeni zake kuhudhuriwa na idadi kubwa ya wananchi.

Akifafanua swali hilo, Lissu alisema chama chake hakijafanya utafiti kujua kama wanaofurika kwenye mikutano hiyo ni wapiga kura, “chama changu hakijafanya utafiti kujua kama hawa wamejiandikisha kupiga kura.”

Akizungumzia uwekaji wa mabango ya wagombea kama ilivyo kwa chama tawala, Lissu amesema chama hicho kinaendelea na michango yake na kwamba, watafanya hivyo nchi nzima.

Hata hivyo, alisisitiza kwamba, mabango hayo kwa kuwa sio ya biashara kwa maana ya kuzalisha pesa, hawatakubali yang’olewe na yaking’olewa watayarudisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!