Friday , 9 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu: …yaani hata sijui
Habari za Siasa

Lissu: …yaani hata sijui

Tundu Lissu, Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chadema
Spread the love

TUNDU Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amesema watu wanaofurika kwenye mikutano yake ya kampeni za urais, hajui kama ni wapiga kura. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza…(endelea).

Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari jijini Mwanza jana Jumamosi tarehe 26 Septemba 2020, Lissu alitoa kauli hiyo alipoulizwa na mwandishi siri ya mafanikio ya kampeni zake kuhudhuriwa na idadi kubwa ya wananchi.

Akifafanua swali hilo, Lissu alisema chama chake hakijafanya utafiti kujua kama wanaofurika kwenye mikutano hiyo ni wapiga kura, “chama changu hakijafanya utafiti kujua kama hawa wamejiandikisha kupiga kura.”

Akizungumzia uwekaji wa mabango ya wagombea kama ilivyo kwa chama tawala, Lissu amesema chama hicho kinaendelea na michango yake na kwamba, watafanya hivyo nchi nzima.

Hata hivyo, alisisitiza kwamba, mabango hayo kwa kuwa sio ya biashara kwa maana ya kuzalisha pesa, hawatakubali yang’olewe na yaking’olewa watayarudisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lussu: Mkataba wa DP bandarini si wa miaka 100

Spread the loveMAKAMU Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, amesema hakuna ukweli wowote...

Habari za SiasaTangulizi

Maulid Mtulia: Kutoka ubunge hadi U-DAS

Spread the love ALIYEKUWA mbunge wa Kinondoni, kupitia vyama vya The Civil...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

error: Content is protected !!