Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu: Nitabadili mfumo
Habari za Siasa

Lissu: Nitabadili mfumo

Tundu Lissu, Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chadema
Spread the love

TUNDU Lissu, mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Tanzania Bara, ameahidi kubadili mfumo wa kibiashara ili kuwaneemesha wananchi waliopo mipakani kiuchumi na kibiashara. Anaripoti Mwandishi Wetu, Karagwe … (endelea).

Akizungumza na wakazi wa Kayanga, Karagwe mkoani Kagera amesema, zipo fursa mbalimbali kwa wakazi wa mipakani na kwamba, miongoni mwao ni kuuza bidhaa ikiwemo mazao nje ya nchi.

Lissu ambaye ni makamu mwenyekiti wa chama hicho amesema, miongo ni mwa mambo yanayorudisha nyuma wakulima ni pamoja na kulazimishwa kuuzia mazao yao vyama vya ushirika.

“Mkulima wa kahawa hapa Karagwe wanaangushwa na vyama vya ushirika. Mkulima akilima mazao yake anaambiwa aweke kwenye gunia kwa kuwa, hawezi kuuza mpaka auzie chama cha ushirika ambacho badala ya kutoa fedha, kinawapa karatasi,” amesema Lissu.

Amesema, tatizo la sasa ni kwamba, wakulima wanalima kahawa yao kwa jasho lao, kisha wanakopwa na hata pale wanapopata malipo ya kahawa yao, bado wanakatwa fedha.

“Mnakopwa kahawa yenu halafu wakija kulipa wanawakata, utaratibu wa kukopa wakulima kahawa umewafanya kuwa masikini,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!