Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu: Hatujidanganyi, uchaguzi huu mgumu
Habari za Siasa

Lissu: Hatujidanganyi, uchaguzi huu mgumu

Tundu Lissu, Mgombea Urais Tanzania (Chadema).
Spread the love

TUNDU Lissu, mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amesema uchaguzi wa mwaka huu ni mgumu. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaaam…(endelea).

Na kwamba, haijawahi kutokea uchaguzi ukawa rahisi lakini huu ni mgumu zaidi akihusisha hali ya kisiasa, mazingira ya upatikanaji wa fedha na miaka mitano ya utawala wa Rais John Magufuli.

Akizungumza na baadhi ya wahariri na waandishi waandamizi wa vyombo mbalimbali vya habari nchini, nyumbani kwake Tegeta, jijini Dar es Salaam leo tarehe 9 Septemba 2020 amesema, kazi ya kuuondoa utawala wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ni kubwa.

“Hatujidangani kwamba kazi ni nyepesi, kazi iliyopo mbele yetu ni kubwa kweli kweli. Nimeshiriki chaguzi tangu mwaka 1995 na mbili nilishinda, nafahamu jinsi uchaguzi wa Tanzania ulivyo mgumu kwa chama chochote cha upinzani.

“Nafahamu ilivyo vigumu kuishinda CCM. Hatujidanganyi kwamba mara hii ikwa rahisi, haijawahi. Mfumo wetu wa uchaguzi umejengwa kuipendelea CCM,” amedai Lissu ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema.

Mgombea huyo ameeleza kuwa, uchaguzi unakuwa mgumu kwa mambo kadhaa akieleza kwamba miongoni mwayo ni watumishi wanaoshughulika na uchaguzi kuwa ‘wateule’ wa mgombea kutoka chama tawala.

Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CCM, John Magufuli akihutubia mkutano wa kampeni Shinyanga

“Mwenyekiti wa tume (Tume ya Uchaguzi) wanateuliwa na rais, msaidizi wake anateule na rais, wasaidizi na wakurugenzi ni wateule wa mgombea wa CCM.

“Wanaweza kuondolewa wakati wowote na rais. Mfumo wa uchaguzi bado ni mgumu, maaskari, usalama na mfumo mzima wa serikali hawapo upande wetu. Tunaamini Watanzania wapo tayari kufanya mabadiliko kweli kweli,” amesema.

Amesema, yeye kama mgombea anaelewa Watanzania wanahitaji ninin kwamba, kikubwa ni kubadilisha mfumo wa kitawala ulioachwa na wakoloni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

Habari za Siasa

ACT Wazalendo yaanika madudu miradi ya ujenzi, moundombinu

Spread the loveCHAMA cha ACT Wazalendo kimeeleza wasiwasi juu ya uelekeo wa...

Habari za Siasa

Samia ashuhudia utiaji saini ujenzi wa minara 758 ya bilioni 265

Spread the love  RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa kampuni za...

error: Content is protected !!