Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif ahofia ‘kukatwa’ urais Z’bar
Habari za Siasa

Maalim Seif ahofia ‘kukatwa’ urais Z’bar

Maalim Seif Sharif Hamad, aliyekuwa Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo
Spread the love

MAALIM Seif Sharif Hamad, mgombea urais Zanzibar katika Uchaguzi Mkuu wa 2020 kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, ameonesha wasiwasi wa kukwamishwa katika kinyang’anyiro hicho. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).

Akizungumza katika Kongamano la Vijana wa ACT-Wazalendo tarehe 8 Septemba 2020 visiwani humo, Maalim Seif amedai, kuna baadhi ya watu wa vyama vingine wamepanga kumuwekea pingamizi katika Tume ya Uchaguzi (ZEC), ili asiteuliwe kugombea.

Amesema, anawakaribisha watu wanaotaka kumuwekea pingamizi akisema, kwamba anafahamu namna ya kupangua pingamizi zao.

Ado Shaibu, Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo akimkabidhi fomu ya kugombea urais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharrif Hamad

“Nasikia kuna watu washapangwa na vyama vingine kuniwekea pingamizi, nawakaribisha kwa sababu kuniwekea pingamizi atakuja kutoa haja zake na ushahidi wake, na mimi naujua vilevile.

“Sioni kama kuna pingamizi yoyote kama itasimama juu yangu. Mimi nimezaliwa Mtambwe, hamjui ninyi? Ndiyo sifa ya kwanza ya mgombea urais awe Mzanzibari wa kuzaliwa sio Mzanzibari mkaribishi,” ameeleza Maalim Seif.

Kwa mujibu wa ratiba ya ZEC, zoezi la uchukuaji na urudishaji fomu  za kugombea urais, lilifunguliwa tarehe 26 Agosti 2020 na linatarajiwa kufungwa leo tarehe 9 Septemba 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!