Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Askofu ahusisha ujenzi wa kanisa na maisha ya jamii
Habari Mchanganyiko

Askofu ahusisha ujenzi wa kanisa na maisha ya jamii

Spread the love

ASKOFU wa Kanisa la Power of God Fire, Dankton Rweikila amesema unapojenga nyumba ya Mungu ni mbegu ambayo inapandwa ndani ya jamii na kusababisha watu kuwa na hofu ya Mungu jambo ambalo linaleta furaha, upendo na amani katika nchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Askofu Rweikila aliyasema hayo Jumapili iliyopita alipokuwa kwenye ibada ya uzinduzi wa ujenzi wa jengo hilo lililopo Chanika Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam.

Alisema jamii inapojenga nyumba ya Mungu inapanda mbegu ambayo kizazi hadi kizazi kinakuwa na hofu ya Mungu ambapo wataogopa kufanya maovu  matokeo yake nchi inakuwa na maendeleo.

Rweikila alisema kanisa linajengwa na mtu anayetambua kuwa Mungu yupo lazima iwe sehemu maalumu ya kumwabudia na yeyote anayejenga nyumba ya Mungu  sadaka ina nguvu katika maisha yake ikiwemo familia, kazi ya mikono na inamlinda kwa kumuepusha na magonjwa,l aana na mauti.

“Mtu anayejitoa kwa hili akatoa sadaka yake, anaandaa ulinzi katika maisha yake hivyo leo tumeweka nguzo kwenye nyumba ya Mungu jambo hili tunamshukuru ametutendea mengi hasa ugonjwa wa corona ametuvusha kuliko nchi zingine,” alisema Rweikila.

Alisema kuna baadhi ya nchi bado zinateseka na ugonjwa huo lakini Tanzania imepata upendeleo wa ajabu ambayo imevushwa pasipo maangaiko yeyote.

Rweikila alisema, Rais John Magufuli akasikia wito ndani yake akatangaza siku tatu ya maombi ambapo kanisa hilo ni miongoni lililoombea Taifa ili liondokane na janga hilo.

Muumini wa kanisa hilo, Getrude Michaila alisema waumini wazidi kujitolea ili kanisa hilo liweze kusimama hivyo wanapojitolea wanapata hazina mbinguni Hadi kizazi na kizazi.

“Tukio la leo linanifundisha mambo mengi ninapanda hii mbegu hadi kizazi changu hivyo familia yangu itakuwa vizuri Kwa kumpendeza Mungu,”alisema Michaila.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!