Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu abadili upepo siasa za CCM
Habari za SiasaTangulizi

Lissu abadili upepo siasa za CCM

Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

SIASA ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) zinazidi kuchukua sura mpya baada ya  kujielekeza kwenye  mashambulizi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

CCM imeanza utaratibu wa kumshambulia Tundu Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki baada ya kuanza kufanya ziara zake Ulaya na Marekani. 

Akiwa ziarani Kilosa, Morogoro Dk. Bashiri Ally, Katibu Mkuu wa CCM amesema kuwa Lissu ‘hajui shida.’

Dk. Bashiru yupo ziarani Morogoro ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha miaka 42 ya kuzaliwa kwa CCM.

Kwenye ziara hiyo juzi Dk. Bashiru alisema, Lissu anadeka huku akimwomba  Rais John Magufuli amtibu.

“Yupo msomi mmoja anaitwa Tundu Lissu ameugua ugonjwa wa deko, anadeka hajui jembe kwa maisha yake, hajui mpunga unalimwaje wala samaki wanavuliwaje.

“Hajapanda bodaboda muda mrefu na watoto wake hawasomi shule hizi anazunguka dunia nzima kutuchafua.

“Tunao Tundu Lissu wengi Serikalini tumewaamini, tumewapa dhamana ila ukiwatembelea ofisini wanadeka,” alisema Dk. Bashiru.

Alisema, Lissu amekuwa akitembea nchi za Ulaya akisema uonga huku akiamini siku moja atakuwa Rais wa Tanzania.

Akiwa ziarani huko Dk. Bashiru amedai kuwa, Lissu anasumbuliwa na ugonjwa wa kusema uongo, deko, uonevu, dharau, kiburi.

“Namuomba Rais wetu aanze kutibu ugonjwa wa deko. Unasomesha watu wanazunguka kutukana nchi yao na Rais wao?” Alieleza kwa kushangaa.

Wakati mtendaji huo wa juu wa CCM akiyasema hayo, Lissu amekuwa akiendeleaa na ziara yake katika nchi za Ulaya ambapo kwa sasa yupo nchini Marekani akieleza ‘hali ya demokrasia nchini’ na kupigwa kwake risasi.

Kutokana na hali hiyo Dk. Bashiru, alisema kuwa dalili za ugonjwa wa aina ya Tundu Lissu ni kusema uongo, dharau, deko, uonevu, kiburi, majivuno.

Amesema kuwa, manesi na madaktari wa ugonjwa huu ni Watanzania nyie wenyewe.

Amesema kuwa, sehemu ya ugonjwa wa Lissu ni kuota urais wa Tanzania, kuwa na kiburi na kwenda Ulaya kuzungumza lugha za wakoloni.

“Lakini sasa anayemwita dikteta amefuta mashamba kwa ajili ya wanyonge,” amesema.

Hata hivyo amesema, watendaji serikali ambao hawataki kupona ugonjwa Wa na Lissu watafute watafute serikali nyingine.

“Ajira ni hiyari, waandike barua waseme chama hiki hakipendi dhuluma, mimi nadhulumu, hakipendi uongo mimi muongo,” Amesema.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!