Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko ‘Limeni kilimo kinachohimili mabadiliko tabia ya nchi’
Habari Mchanganyiko

‘Limeni kilimo kinachohimili mabadiliko tabia ya nchi’

Shamba la mihogo
Spread the love

WAKULIMA nchini wametakiwa kutumia ardhi ndogo ya kilimo waliyonayo, kuzalisha kwa tija na kufikia malengo ya kilimo kinachohimili mabadiliko ya tabia nchi (CSA). Anaripoti Christina Haule, Morogoro … (endelea).

Mtafiti mwandamizi kutoka Taasisi ya Kimataifa ya Kilimo cha Kitropiki (IITA), Dk. Freddy Baijukya ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari za Kilimo, Sayansi na Teknolojia Tanzania (TAJF), uliofanyika kwa ufadhili wa Shirika la Msaada la Marekani (USAID).

Dk. Baijukya amesema, matumizi ya ardhi ndogo kwa kilimo chenye tija yatasaidia mkulima kuweza kuzalisha mazao, ikiwemo mahindi kwa wastani wa tani 2.5 kwa hekta kiasi ambacho hakijafikiwa hata nusu yake mpaka sasa. 

Amesema, wamejipanga kuelimisha wakulima juu ya CSA inavyoangalia na kuondoa madhara yatokanayo na mabadiliko ya tabia nchi na kuongeza uzalishaji wenye tija.

Pia kuzingatia uvumilivu kwenye mabadiliko ya tabianchi sambamba na kupunguza uzalishaji wa gesi za kijani, ikiwemo gesi ya ukaa jambo litakalomsaidia mkulima.

Na kwamba, licha ya ufugaji na kilimo kuonekana chanzo cha mabadiliko ya tabia nchi, lakini ndio sehemu ya uti wa mgongo wa uchumi wa nchi hivyo, ni vema malengo na sera yaliyowekwa na Serikali yaweze kutekelezeka.

“Mfano eneo la Iringa uzalishaji wa zao la Pamba umeshuka kutokana na wanawake kususa kupalilia, kwasababu wanaume wanalala hoteli miezi mitatu baada ya mauzo na kurejea nyumbani wakiwa hawana kitu,” alisema.

Dk. Baijukya amesema, kumsaidia mwanamke kuendeleza kilimo kunaweza kufanikiwa kwa kuleta mashine rahisi zitakazomsaidia na hivyo kumpa nguvu ya kuendeleza kilimo nchini.

Mwakilishi wa Wizara ya Kilimo Kitengo cha Mazingira, Evelyn Kagoma amesema wizara imeendelea kuandaa sera na mipango mbalimbali ya kusaidia wakulima, ikiwemo kufanya urutubishaji wa ardhi na upatikanaji wa maji kwenye maeneo ya kilimo.

Aliitaja mipango mingine kuwa ni kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi, kwa kufuata mwongozo wa kuhimili athari za mabadiliko ya tabia nchi uliozinduliwa rasmi mwaka 2017.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

Habari Mchanganyiko

Somo la dini: Waislamu waishukia Serikali, wizara yatoa kauli

Spread the loveJUMUIYA na Taasisi za Kiislamu Tanzania, imetupia lawama Serikali ikidai...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!