Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lijuakali ajivunia kuijenga Chadema
Habari za SiasaTangulizi

Lijuakali ajivunia kuijenga Chadema

Peter Lijualikali, aliyekuwa Mbunge wa Kilombero
Spread the love

PETER Lijuakali, mwanachama mpya wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), amesema Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kilipaswa kumshukuru kwa kuwa ndiye aliyekijenga Kilombero, Morogoro. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro … (endelea).

Akizungumza na kituo kimoja cha redio nchini leo tarehe 23 Julai 2020 amesema, kama Chadema imemtoa mbali, basi na yeye ameitoa Chadema mbali hivyo wametoana mbali.

Amesema, Chadema haikuwa kwenye ramani ya wakazi wa Kilombero na kwamba, kauli kuwa yeye ndiye anayepaswa kukishukuru chama hicho haina maana.

        Soma zaidi:-

“Mimi nimefanya mambo ambayo yameiweka Chadema kwenye ramani Kilombero, moyo wangu, mikakati yangu, akili yangu, ushupavu wangu ndio zimefanya Chadema imekaa kwenye ramani ambayo ipo pale,” amesema Lijualikali

Mwanasiasa huyo kijana ni miongoni mwa waliokuwa wabunge wanaotokana na Chadema, alihama chama hicho na kujiunga na CCM, hata hivyo ameshindwa kupenya mbele ya mtia nia mwenzake Abubakari Asenga katika jimbo hilo la Kilombero.

Peter Lijualikali (kushoto) akipokea fomu ya kuwania ubunge jimbo la Kilombero kwa tiketi ya CCM

Amesema, kwenye tatizo kubwa lilijikita kwenye mtazamo wa kutoana mbali “hapa ndipo palipo na tatizo. Wanaohama CCM kwenda vyama vingine hawaambiwi wewe tumekutoa mbali.”

Amedai, dhana ya kutoana mbali ilianzishwa ndani ya chama hicho ili kuzima hisia za kuhoji baadhi ya mambo ambayo yalionekana kutokwenda sawa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!