Saturday , 4 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Kundi la tano kaya 25 kutoka Ngorongoro mbioni kuhamia Msomera
Habari Mchanganyiko

Kundi la tano kaya 25 kutoka Ngorongoro mbioni kuhamia Msomera

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu- Sera, Bunge na Uratibu nchini Tanzania, Balozi Pindi Chana
Spread the love

 

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Balozi Pindi Chana amesema kundi la tano la wakazi wa Ngorongoro takribani kaya zisizopungua 25 kwa sasa lipo kwenye mchakato wa kuhama kwenda Msomera mkoani Tanga kwa hiari. Anaripoti Apaikunda Mosha, TUDARCo … (endelea).

Amesema hayo leo Ijumaa ya tarehe 19 Agosti 2022, katika hafla ya kuhamisha wananchi wa Ngorongoro awamu ya pili Kwenda Msomera kwa hiari kwa lengo la kuiacha Ngorongoro ibaki kama eneo la hifadhi kwa ajili ya maslahi ya Taifa.

Amebainisha kuwa shughuli za uhifadhi zinachangia takribani asilimia 17 ya pato la taifa na asilimia 25 ya mapato ya nje, ambapo inasaidia kuleta maendeleo kama ujenzi wa miundombinu ikiwemo elimu na afya.

Amesema kuwa kitendo cha wananchi hao kukubali kwa hiari kuhama kitawanufaisha kwani kwa kuzingatia haki za wananchi hao watajipatia haki zao za msingi ikiwemo umiliki wa ardhi ambapo katika eneo la hifadhi wananchi hawaruhusiwi kumiliki ardhi.

Pia ameeleza kuwa wananchi watajipatia maendeleo ya elimu ikiwemo ujenzi wa shule, vyuo vikuu na VETA.

Amethibitisha kuwa zoezi hilo linaendelea vizuri kwani upo utaratibu mzuri wa kusafirisha watu na mifugo. Pia miundombinu pamoja na nyumba zipo tayari katika eneo la Msomera.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua huduma maalum kwa wastaafu

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua huduma maalum kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yazindua akaunti ya Kikundi

Spread the loveBenki ya NMB imezindua akaunti ya kikundi yenye  maboresho makubwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

error: Content is protected !!