Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Ukraine yahofia Urusi kuzima kinu cha kufua umeme cha nyuklia
Kimataifa

Ukraine yahofia Urusi kuzima kinu cha kufua umeme cha nyuklia

Spread the love

KAMPUNI ya nyuklia ya serikali ya Energoatom ya Ukrein imesema vikosi vya Urusi vilipanga kuzima mtambo wa kuendesha umeme kwenye mtambo wa nyuklia wa kuzalisha umeme wa Zaporizhzhia na kuutenganisha na gridi ya nishati ya Ukraine. Anaripoti Apaikunda Mosha, TUDARco kwa msaada wa mashirika ya kimataifa … (endelea).

Katika taarifa yake, Energoatom imesema inaaminika kuwa Urusi ambavyo inadhibiti mtambo wa kuzalisha umeme katika eneo la Ukraine Kusini ilikuwa inajiandaa kufanya ‘’chokozi kubwa’’ huko. Moscow yenyewe iliishutumu Kyiv kwa kufanya “uchochezi” kwenye tovuti siku ya Alhamisi.

“Kuna habari kwamba vikosi vya uvamizi vya Urusi vinapanga kuzima vizuizi vya umeme na kutenganishwa kutoka kwa njia za usambazaji wa umeme hadi kwa mfumo wa umeme wa Ukraine hivi karibuni”, taarifa ya Ukraine imesema.

“Jeshi la Urusi kwa sasa linatafuta wasambazaji wa mafuta ya jenereta za dizeli, ambazo zinapaswa kuwashwa baada ya vitengo vya umeme kuzimwa kwa kukosekana kwa usambazaji wa umeme wa nje wa mfumo wa kupozea mafuta ya nyuklia,” imesema.

Mtambo mkubwa wa kuzalisha umeme wa nyuklia, Mkubwa zaidi barani Ulaya, ulitekwa na vikosi vya Urusi mnamo Machi, lakini bado unawafanyakazi wabobezi wa Ukraine, ingawa ni wawili tu walioguswa kati ya sita wanaofanya kazi kwa uwezo kamili.

Kuzimwa kwa mtambo huu kunaweza kuleta shinikizo jipya kwa usambazaji wa Ukraine, hasa Kusini. Ukraine tayari inajiandaa kwa msimu wake wa baridi mgumu zaidi tangu uhuru na inajiandaa kwa uhaba wa nishati unaowezekana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!