Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kuelekea Oktoba 2020; wanasiasa waanza kutuhumiana
Habari za Siasa

Kuelekea Oktoba 2020; wanasiasa waanza kutuhumiana

Spread the love
TUHUMA kwamba, baadhi ya vyama vya siasa vimenza kuandaa vijana kwa ajili ya vurugu, kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba 2020, zimetolewa bungeni. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Naftaha Nachuma, Mbunge wa Mtwara Mjini (CUF) amedai, baadhi ya viongozi wa  vyama vya siasa, wameanzisha vikundi vya uhalifu kwa ajili ya kufanya fujo katika uchaguzi huo.

Nachuma ametoa madai hayo leo tarehe 4 Februari 2020, wakati akiuliza swali bungeni jijini Dodoma. Lililohoji mkakati wa serikali katika kukabiliana na changamoto ya uvunjifu wa amani kwenye uchaguzi huo.

Mbunge huyo wa CUF amemueleza  Mhandisi Hamad Masauni, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, kwamba ana ushahidi juu ya swala hilo, na kumtaka aende Mtwara kuchukua ushahidi huo

“…pamoja na majibu mazuri nina maswali mawili , la kwanza hivi sasa Mtwara,  Manispaa ya Mtwara Mikindani kuna baadhi ya viongozi wa siasa ambao wameweza kuratibu vikundi mbalimbali kwa ajili ya kufanya vurugu katika uchaguzi wa  2020, yuko tayari kuja Mtwara kuchukua ushahidi ambao nitampatia kwa mikono yangu,” amehoji Nachuma.

Akijibu swali hilo, Mhandisi Masauni amesema yuko tayari kuchukua ushahidi huo

“Swali lake la kwanza ameuliza kama niko tayari, niko kufanya hivyo kama ushahidi anao,” amejibu Mhandisi Masauni.

Wakati huo huo, Mhandisi Masauni amesema Serikali kupitia Jeshi la Polisi linanoa askari wake ili waweze kukabiliana na vitendo vinavyohatarisha usalama wa nchi kwenye uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika mwezi Oktoba mwaka 2020.

Mhandisi Masauni amesema kwa sasa askari hao wanapewa mafunzo ya ukakamavu na upelelezi, pia serikali imewaongezea vifaa vya utendaji kazi.

“Serikali kupitia Jeshi la Polisi  inaendelea kutoa mafunzo mbalimbali ya kwa askari wake, ya ukakamuavu, upelezi na kuongeza vifaa vya kutendea kazi ili kuwajengea uwezo na ueledi mkubwa wa kuzuia na kukabiliana na vitendo hivyo vinavyojitokeza nyakati za uchaguzi,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!