KIKAO cha Bunge kilichokuwa kinaendelea leo Jumanne, tarehe 27 Juni 2023, kimeahirishwa ghafla baada ya kutokea dharura. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).
Kikao hicho cha 56 cha mkutano wa 11 wa Bunge la 12, kimeahirishwa na Spika Dk. Tulia Ackson, baada ya kengele ya dharura kulia wakati Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, anajibu maswali ya wabunge.
Baada ya kengele hiyo kulia, Spika Tulia alimkatisha Mhandisi Kasekenya, na kuwaelekeza wabunge watoke nje ya ukumbi wa bunge hadi dharura hiyo itakapopatiwa ufumbuzi.
“Naibu waziri na wabunge nadhani hiyo inaashiria tutoke humu ndani kwa haraka, kila mtu afuate mlango ulio karibu yake haraka tutoke. Sote twende sehemu ile ya kukusanyika watu, naahirisha mpaka jambo hili litakaporekebishwa,” amesema Spika Tulia.
Leave a comment