Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi ya Mbowe; Jamhuri yapinga nyaraka za utetezi zisipokelewe na mahakama
Habari za Siasa

Kesi ya Mbowe; Jamhuri yapinga nyaraka za utetezi zisipokelewe na mahakama

Spread the love

 

MAWAKILI wa Jamhuri katika kesi ya ugaidi imayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake, wamepinga upokeaji wa nyaraka za upande wa utetezi, katika kesi ndogo ya kupinga maelezo ya onyo ya mshtakiwa wa tatu, Mohammed Andillah Ling’wenya. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Mawakili hao wameweka pingamizi hilo leo Jumanne, tarehe 30 Novemba 2021, kwenye Mahakama Kuu, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Mawasiliano Dar es Salaam, mbele ya Jaji Joachim Tiganga.

Baada ya shahidi wa pili wa upande wa utetezi katika kesi hiyo ndogo, Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), mkoani Kilimankaro, Lembrus Mchome, jana kuiomba mahakama hiyo izipokee nyaraka hizo kwa ajili ya kielelezo.

Nyaraka hizo ni, barua ya Wakili Peter Kibatala, kwenda kwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kuomba mwenendo wa kesi iliyokuwa inamkabili mahakamani hapo, nyaraka yenye taarifa za mwenendo wa kesi hiyo, dispach na hati ya mshtaka.

Upande wa Jamhuri ukiongozwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Robert Kidando, uliweka pingamizi dhidi ya upokeaji nyaraka hizo ukidai shahidi anayetaka kuzitoa hana uwezo, pia nyaraka husika hazina umuhimu.

Wakili Kidando amedai wanapinga upokeaji wa nyaraka hizo kwa kuwa hazina umuhimu kwenye mwenendo wa kesi hiyo ndogo.

“Tuna mapingamizi kuhusiana na upokeaji wa nyaraka hizo zinazotaka kutolewa na shahidi wa pili. Tumegawa mapingamizi yetu kama ifuatavyo, pingamizi la kwanza kuhusu mwenendo wa kesi, charge sheet (hati ya mashtaka) pamoja na barua inayodaiwa kuandikwa kwenda kwa Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, nyaraka hizi hazina relevance (umuhimu) katika proceeding zinazoendelea dhidi ya mshtakiwa wa tatu,” amedai Wakili Kidando.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!