MAHAKAMA Kuu, kanda ya Dar es Salaam, inatarajiwa kutoa maamuzi muda mfupi ujao, iwapo maombi ya Freeman Mbowe na Ester Matiko ya kupewa dhamana yaendelee kusikilizwa ama yasubiri maamuzi ya rufaa yaliyowasilishwa na serikali kupinga kutupwa kwa mapingamizi yao. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Wakili wa Serikali Mkuu, Paul Kadushi ameieleza Mahakama Kuu leo Ijumaa Novemba 30, 2018 kuwa baada ya kukata rufaa kwa sasa Mahakama Kuu haina mamlaka ya kuendelea na usikilizwaji wa rufaa hiyo ya kina Mbowe.
Hata hivyo, kumeibuka malumbano baina ya mawakili wa pande zote, huku mawakili wa kina Mbowe wakipinga uhalali wa taarifa ya Serikali ya kusudio la kukata rufaa kwa madai hawajafahamishwa na Msajili wa Mahakama Kuu kuhusu kuwepo kwa taarifa hiyo.
Kwa habari zaidi, soma MwanaHALISI Online.
Leave a comment