
Spread the love
MAHAKAMA Kuu, Kanda ya Dar es Salaam, imekubaliana na maombi ya Jamhuri ya kughairisha usikilizaji wa rufaa ya mwenyekiti wa Chadema, Freman Mbowe na Mbunge wa Tarime, Ester Matiko. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Maamuzi hayo yametolewa muda mfupi uliopita mahakamani hapo na Jaji Sam Runyamika anayesikiliza shauri hilo.
Kabla ya kufikia maamuzi hayo, Jaji Runyamika alitoa nusu saa kuamua, iwapo maombi ya Mbowe na Matiko ya kupewa dhamana yaendelee kusikilizwa ama yasubiri maamuzi ya rufaa.
Serikali iliwasilishwa mahakamani muda mfupi kupinga usikilizaji wa shauri hilo hadi rufaa yao itakaposikilizwa.
More Stories
Chadema yatangaza mchakato mrithi wa Halima Mdee
Mkurugenzi Jiji la Dar, ahamishiwa Kinondoni
Sita wadakwa kwa utakatishaji fedha Bil 4.78