Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kero Daraja Mto Buhu kumalizwa
Habari Mchanganyiko

Kero Daraja Mto Buhu kumalizwa

Mwita Waitara
Spread the love

 

GHARAMA za ujenzi wa Daraja la Mto Buhu (Munguri B), lililopo Kondoa, mkoani Dodoma, zitaingizwa katika bajeti ya Mwaka wa Fedha 2021/22. Anaripoti Jemima Samwel, DMC … (endelea).

Ni kauli ya Mwita Waitara, Naibu wa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, aliyoitoa leo tarehe 3 Mei 2021, jijini Dodoma wakati akijibu swali la Ally Makoa, Mbunge wa Kondoa mjini (CCM).

Makoa alitaka kujua, kwamba lini serikali itaanza kujenga daraja hilo ili wananchi wa upande wa pili wa mto waweze kuvuka na kupata huduma mbalimbali za kijamii upande mwingine.

“Kwa kutambua changamoto hii, wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), imetenga fedha katika bajeti ya mwaka wa fedha 2020/21 kwa ajili ya kufanya usanifu wa Daraja jipya katika Mto Bubu,” amesema Waitara.

Amefafanua, daraja hilo lipo katika Barabara ya Kondoa – Nunguri – Mtiriangwi – Gisambalang – Nangwa, lenye jumla ya urefu wa Km 81.4 na kwamba, barabara hiyo inaunganisha Mkoa wa Dodoma na Manyara kupitia Wilaya za Kondoa na Hanang’.

“Mvua kubwa zilizonyesha mwaka 2019/20, zilisababisha Mto Bubu kutanuka na kufanya Daraja la Munguri B kutopitika wakati wa mvua.

“Taratibu za ununuzi wa kumpata Mhandisi Mshauri zipo katika hatua za mwisho ambapo kazi hiyo inatarajiwa kuanza Juni, 2021,” amesema.

Amesema, katika mapendekezo ya bajeti ya mwaka wa fedha 2021/22, daraja hili limetengewa Sh. 66 milioni kwa ajili ya kukamilisha kazi ya usanifu, na baada ya usanifu kukamilika, ujenzi wa daraja hilo utaanza kulingana na upatikanaji wa fedha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!