Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Mil 250 kukamilisha zahanati Minyeye, Mnung’una, Msikii
Elimu

Mil 250 kukamilisha zahanati Minyeye, Mnung’una, Msikii

Dk. Festo Dugange, Naibu Waziri Ofisi ya Rais
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imetenga Sh. 250 milioni kwa ajili ya kukamilisha maboma matano ya Zahanati ya Minyeye, Mnung’una na Msikii katika Wilaya ya Singida, Anaripoti Jemima Samwel DMC …(endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo Jumatatu Tarehe 3 Mei 2021, na Dk. Festo Dugange, Naibu Waziri Ofisi ya Rais katika kipindi cha maswali na majibu bungeni, jijini Dodoma wakati akijibu swali la Abeid Ramadhani, Mbunge Singida Kaskazini (CCM).

“Je, ni lini serikali itamaliza ujenzi wa maboma ya Vituo vya Afya yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi katika Kata za Makuro na Ngimu?” amehoji.

Akijibu swali hilo, Dk. Dugange amesema, ili kuboresha huduma za afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Singida, katika mwaka wa fedha 2018/19 serikali iliipatia wilaya hiyo Sh. 1.5 Bilioni kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya halmashauri.

“Katika mwaka wa fedha 2020/21, hospitali hiyo ilitengewa Sh. 500 Milioni kwa ajili yaujenzi wa wodi tatu na Sh. 500 Milioni kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba.”

“Pia, katika mwaka wa fedha 2021/22 serikali imetenga Sh. 250 Milioni kwa ajili ya kukamilisha maboma ya Zahanati ya Minyeye, Mnung’una na Msikii katika Halmashauri ya Wilaya ya Singida,” ameeleza Kandege.

Amesema, serikali itaendelea kujenga, kukarabati, kupanua na kukamilisha maboma ya miundombinu ya kutolea huduma za afya nchini yakiwamo maboma ya vituo vya afya katika Kata za Makuro na Ngimu, kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

error: Content is protected !!