WAKATI Chama cha ACT-Wazalendo kikitangaza nia ya kujiondoa kwenye Serikali ya Umoja wa Kitaifa – Zanzibar (SUK), Rais Mstaafu wa Zanzibar Amani Abeid Karume amewataka viongozi wa pande zote kukaa chini kuzungumza. Anaripoti Faki Sosi …(endelea).
Akihojiwa na UTV Visiwani Zanzibar, Karume amesema kuwa kitendo cha viongozi kutaka kujiondoa kwenye serikali ni kukimbia majukumu yao.
“Hapo nyuma yalishatokea matatizo makubwa kuliko haya tukasema tukae chini yakazungumzwa” amesema Karume.
Karume amesema kuwa suluhu ya matatizo yote ni watu kukaa chini kuzungumza kwa pamoja “Wakae chini wazungumze watafute suluhisho”
Leave a comment