Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kamati ya Bunge yatoa mapendekezo manne changamoto ukosefu ajira kwa vijana
Habari za Siasa

Kamati ya Bunge yatoa mapendekezo manne changamoto ukosefu ajira kwa vijana

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki akikabidhi madume ya ng'ombe kwa wafugaji wa Maswa
Spread the love

 

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, imetoa mapendekezo manne kwa Serikali, juu ya namna ya kutatua changamoto za ukosefu wa ajira kwa vijana. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Mapendekezo hayo yamewasilishwa bungeni jijini Dodoma, leo tarehe 8 Februari 2023 na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, Joseph Mhagama, akiwasilisha taarifa ya shughuli za kamati hiyo kwa kipindi cha kuanzia Februari 2022 hadi Januari 2023.

“Kamati inatambua kwamba, ukosefu wa ajira hasa kwa vijana ni changamoto ambayo ina athari kijamii na kiuchumi na kwa kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu ina wajibu wa kuratibu utekelezaji wa sera, sheria na mikakati ya kukuza ajira na kutoa huduma za ajira, ili kuongeza nafasi za ajira kwa watanzania ndani na nje ya nchi,” amesema Mhagama.

Mhagama ametaja mapendekezo hayo kuwa ni, Serikali kuongeza jitihada za kusimamia sera na sheria mbalimbali zinazoweka mazingira bora ya uwekezaji kwenye sekta zenye uwezo mkubwa wa kuzalisha ajira ikiwemo kilimo, ufugaji, uvuvi na biashara.

Pendekezo lingine ni, Serikali kuhamasisha uwekezaji katika viwanda vidogo, vya kati na vikubwa ili viweze kuajiri sehemu kubwa ya nguvu kazi nchini na vijana wengine kujiajiri wenyewe, huku lingine likiwa ni kubuni utaratibu madhubuti wenye uwazi ambao utaratibu zoezi zima la ajira Serikalini kwa namna ambayo, nafasi zitakozajazwa zitaakisi umoja wa kitaifa, bila kuathiri vigezo.

“Kuwa na mpango wa kuhamasisha vijana nchini kujifunza stadi za kazi za kimkakati na baadae kuwaunganisha vijana hao na fursa za kazi zenye staha nje ya nchi, kulingana na ushindani wa soko la ajira la kimataifa katika sekta za mbalimbali kwa kushirikiana na balozi zetu,” amesema Mhagama.

Katika hatua nyingine Mhagama amesema, kamati hiyo inaishauri Serikali kuweka mikakati ya utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana ya 2007, ili kuwawezesha vijana katika utekelezaji wa masuala ya maendeleo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!