Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kamati ya Bunge yaonesha huruma kwa wananchi  
Habari za Siasa

Kamati ya Bunge yaonesha huruma kwa wananchi  

Spread the love

WABUNGE wamejadili na kupitisha miswada miwili ukiwamo wa Sheria ya Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Ardhini, huku kamati ya Bunge ikikataa kiwango cha adhabu na vifungo vikubwa kwenye sheria hiyo na kushauri vipunguzwe ili kuendana na hali halisi. Anaripoti Danson Kaijage…(endelea).

Viwango vya tozo vinavyopigiwa kelele ili vipunguzwe ni vile vinavyohusu adhabu kwa watumiaji wa huduma za usafiri wa ardhini.

Muswada huo una kifungu cha 42 (1) na (2) kinachotoa adhabu kubwa ya faini na kifungo kwa mtu aliyetenda kosa cha Sh. 3,000,000 kwa mtu mmoja na Sh. 5,000,000 kwa kampuni au kifungo cha miaka miwili jela au vyote kwa pamoja.

Akiwasilisha maoni na ushauri wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundo Mbinu kuhusu muswada huo leo tarehe 30 Januari 2019, Dk. Chuachua Mohamed Rashid amesema, kamati hiyo inaona asilimia 1.5 inayotozwa kwenye pato ghafi ni kiwango kikubwa sana, kwani wakati mwingine unaweza kukusanya kiasi kingi, lakini kwa uhalisia hakuna faida kubwa.

Kwa mujibu wa Chuachua, kamati yao inapendekeza kiwango hicho cha asilimia 1.5 kirekebishwe na kiwe asilimia moja kwenye kifungu cha 35 (3) ambacho kinazungumzia tozo katika sheria hiyo.

“Katika maoni yetu ya jumla, kamati inaona viwango vya tozo za watoa huduma kubadilisha tozo ni mlolongo mrefu na kwa muda mrefu viwango hivyo havijafanyiwa marekebisho.

“Tunashauri katika kanuni kuwe na kikokotoo kinachotokana na gharama ya uendeshaji ili kutatua changamoto hii,”amesema.

James Mbatia, Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni akiwasilisha maoni na ushauri kuhusu tozo na adhabu mbalimbali zilizotajwa katika muswada huo, amesema lengo la muswada huo lisiwe ni kuwatesa au kuwapa adhabu watumiaji wa huduma za usafiri wa ardhini.

Katika muswada huo, Mbatia alianza kwa kuunga mkono serikali kuleta bungeni muswada huo akidai kuwa una maslahi mapana kwa taifa na wala wao hawaupingi.

“Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inashauri kwamba adhabu ni kubwa mno na kinatoa taswira ya kukomoa badala ya kurekebisha tabia.

“Kwa ajili ya kuweka mazingira rafiki ili watu wote waweze kunufaika na mwenendo wa soko na kuondoa uwezekano wa baadhi ya watu kuhodhi mwenendo wa soko na ni vyema serikali iweke utaratibu wa kulinda wadau wote,” amesema Mbatia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!