Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM awatumbua RC Gambo, DC na DED Arusha
Habari za Siasa

JPM awatumbua RC Gambo, DC na DED Arusha

Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa viongozi watatu wa Mkoa wa Arusha na kufanya uteuzi wa viongozi watakaoshika nyadhifa hizo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea)

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa leo Ijumaa usiku tarehe 19 Juni 2020 imeelezea mabadiliko hayo.

Kwanza, Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo na amemteua Idd Kimanta kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Kabla ya uteuzi huo, Kimanta alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha.

Nafasi ya Mkuu wa Wilaya ya Monduli itajazwa baadaye.

Pili, Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Arusha(DC), Gabriel Daqarro na amemteua, Kenan Kihongosi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha.

Kabla ya uteuzi huo, Kihongosi alikuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Iringa.

Tatu, Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Halmashauri ya Jiji la Arusha (DED) Dk. Maulid Madeni na amemteua Dk. John Pima kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha.

Kabla ya uteuzi huo, Dk.Pima alikuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua Mkoani Tabora.

Aidha, Rais Magufuli amemteua, Jerry Mwaga kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua.

Kabla ya uteuzi huo, Mwaga alikuwa Afisa katika Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wateule wote wanatakiwa kuwepo Ikulu Jijini Dar es Salaam, Jumatatu tarehe 22 Juni, 2020 saa 2:30 asubuhi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!