Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Profesa Ndalichako atoa maagizo Chuo cha Ualimu Mpwapwa
Elimu

Profesa Ndalichako atoa maagizo Chuo cha Ualimu Mpwapwa

Spread the love

WAZIRI wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako ameuagiza uongozi wa Chuo cha Ualimu Mpwapwa jijini Dodoma, kuhakikisha miundombinu ya chuo hicho inalindwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mpwapwa … (endelea).

Hayo ameyasema jana Ijumaa tarehe 19 Juni 2020 alipokagua maendeleo ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu katika chuo hicho ambao umegharimu zaidi ya  Sh. 2.8 bilioni.

Akizungumza na wakufunzi, walimu na wanafunzi wa chuo hicho, Profesa Ndalichako alisema, Serikali imeamua kuwekeza katika uboreshaji wa miundombinu ya Taasisi za Elimu ili kuongeza fursa ya upatikanaji wa elimu kwa Watanzania.

Alitaja miundombinu inayojengwa ni jengo moja la ghorofa kwa ajili ya Idara ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), Bweni la ghorofa moja la walimu tarajali wa kike, bwalo la chakula na nyumba mbili za watumishi ambazo nyumba moja ina uwezo wa kuchukua familia tatu. 

“Serikali imeamua kwa dhati kuboresha miundombinu ya elimu ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kunakuwa na upatikanaji wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia ndio maana inawekeza katika eneo hili.”

“Sasa ni jukumu lenu kusimamia na kuhakikisha miundombinu inatunzwa ili iweze kutumika kwa muda mrefu,” alisema Waziri Ndalichako.

Naye Kaimu Katibu Tawala, Said Mwaliego akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Jabili Shekimweri, aliishukuru Wizara kwa kupeleka kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa chuo hicho. 

Aliiomba Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kusimamia mradi huo kwa karibu ili ukamilike kwa wakati. 

Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo cha Ualimu Mpwapwa, Gerald Richard aliishukuru wizara kwa kukipatia fedha za ukarabati chuo hicho kwani miundombinu yake ilikuwa imechakaa kutokana na kuwa cha muda mrefu.

Alisema ujenzi wa miundombinu unaoendelea utaongeza nafasi za udahili wa wanachuo wengi zaidi.

1 Comment

  • Nilikuwa naomba nafasi ya kujiunga na mafunzo ya ualimu mpwapwa nimemaliza form four 2019

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

RC Songwe ang’aka kesi 2 kati ya 60 za mafataki kuamuliwa

Spread the loveMkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael ameshangazwa na...

error: Content is protected !!