Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko JPM atuma salamu za rambirambi vifo vya watu 19 Songwe
Habari Mchanganyiko

JPM atuma salamu za rambirambi vifo vya watu 19 Songwe

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli ametuma salamu za rambirambi kwa familia zilizopoteza ndugu na jamaa zao katika ajali ya barabara iliyotokea wilayani Mbozi mkoa wa Songwe jana tarehe 21 Februari 2019.Anaripoti Bupe Mwakiteleko…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa, Rais Magufuli amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Songwe , Brigedia Jenerali,Mstaafu, Nicodemas Mwangela kufikisha salamu zake zza pole kwa familia hizo.

Aidha, Rais Magufuli amezitaka mamlaka zinazohusika na usalama wa barabarani mkoani Songwe kufanya uchunguzi wa ajali hiyo na kuchukua hatua zinazostahili pamoja na kujipanga vizuri kukabiliana na matukio ya ajali za barabarani.

Ajali hiyo ilitokea majira ya saa tatu na robo usiku katika mteremko wa Senjele ambapo Lori lililokuwa linatokea Tunduma kwenda Mbeya Mjini liligonga basi la abiria kwa nyuma, kisha basi hilo na kusababisha vifo vya watu 19.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli ametoa mkono wa pole kwa familia ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla ambaye amefiwa na mtoto wake, Zul Hamis Kigwangalla jana tarehe 21 Februari 2019.

“Rais Magufuli akiwa na mkewe, Mama Janeth Magufuli wamefika nyumbani kwa familia hiyo Mikocheni jijini Dar es Salaam na kukutana na baadhi ya wanafamilia wakiongozwa na mama wa marhemu, Dk. Bayoum Kigwangalla wakiwa katika maandalizi ya kusafirisha mwili wa marehemu kwenda Nzega mkoani Tabora,” inaeleza sehemu ya taarifa ya Msigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!