Tuesday , 3 October 2023
Home Habari Mchanganyiko Waliochoma Kituo cha Polisi  Bunju A wafungwa maisha
Habari Mchanganyiko

Waliochoma Kituo cha Polisi  Bunju A wafungwa maisha

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam leo tarehe 22 Februari 2019 imewafunga maisha jela watu wanane baada ya kukutwa na hatia katika kesi ya kuchoma moto Kituo cha Polisi cha Bunju A kilichopo jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hukumu hiyo iliyoacha simanzi imetolewa leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Simba amesema kitendo cha watu hao kuchoma kituo hicho hakivumiliki na kushindwa kuwaonea huruma kutokana na kuhatarisha usalama wa nchi.

Washtakiwa hao walitekeleza tukio hilo tarehe 10 Julai mwaka 2010, ambapo walikuwa wanakabiliwa na mashtaka sita ikiwemo shtaka hilo la kuchoma moto kituo hicho.

Mbali na washtakiwa hao nane kufungwa maisha jela, Mahakama imewaacha huru watu 10  walioshtakiwa kwa kosa hilo. Awali wakati kesi hiyo inafunguliwa, kulikuwa na washtakiwa 35 ambapo 17 waliachwa huru na kubaki 18, ambapo leo hii kumi waliachwa huru pia baada ya kuonekana hawana hatia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wawili wanaswa wakitengeneza noti bandia

Spread the loveJESHI la Polisi mkoani Songwe limewakamata watu wawili kwa tuhuza...

AfyaHabari Mchanganyiko

Chanjo mpya ya malaria Sh 5,000-10,000

Spread the loveShirika la afya la Duniani (WHO) limeridhia chanjo ya pili...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wagonjwa kiharusi waongezeka, Hospitali Mkapa yaja matibabu mapya

Spread the loveHOSPITALI ya Benjamini Mkapa kwa kushirikiana na madaktari Bingwa kutoka...

Habari Mchanganyiko

Wananchi waamua kujenga zahanati kukwepa adha kufuata huduma mbali

Spread the loveWANANCHI wa Kijiji cha Kwikerege, kilichopo katika Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!