SAFARI ya miaka 10 ya ndoa ya Suzana Ndaga Mtuwa na Denis Mtuwa iliyofungwa katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Kimara jijini Dar es Salaam, imehitimishwa Jumapili tarehe 21 Machi 2021. Anandika Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).
Ni baada ya Suzana, watoto wake wawili wa kuwazaa na wawili wa shemeji zake kukanyagwa na kufariki dunia wakati wa kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa Tanzania, John Magufuli katika Uwanja wa Uhuru, mkoani Dar es Salaam.
Wanafamilia hao walitoka alfajiri ya saa 11 na kuanza safari ya kwenda kumuaga Dk. Magufuli, lakini hawakurejea tena nyumbani.
Gerard Mtuwa ambaye ni kaka wa Denis anasimulia mkasa ulivyokua, fuatana na MwanaHalisi TV katika simulizi hii ya kusikitisha..
Leave a comment