Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mwili Magufuli wawasili Z’bar, Uwanja wa Aman wafurika
Habari za SiasaTangulizi

Mwili Magufuli wawasili Z’bar, Uwanja wa Aman wafurika

Spread the love

 

WANANCHI wa Zanzibar, wamejitokeza kwa wingi kuuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati John Pombe Magufuli, aliyefariki dunia tarehe 17 Machi 2021. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), aina ya Air Bus, iliyobeba jeneza lenye mwili wa Dk. Magufuli, iliruka Uwanja wa Ndege wa Dodoma saa 2:40 asubuhi na kutua Uwanja wa Abeid Aman Karume saa 3:20 asubuhi. Ikiwa imetumia dakika 40.

Viongozi mbalimbali wamejitokeza kuupokea uwanjani hapo wakiongozwa na Rais wa Zanzibar, Hussein Ali Mwinyi na Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa.

Makamu wa Kwanza wa Rais, Othuman Masoud Othuman, Makamu wa Pili wa Rais, Hemed Suleiman Abdulla, mawaziri, watendaji mbalimbali wa Serikali na sekta binafsi.

Uwanja wa Aman, maelfu ya wananchi wamejitokeza tangu asubuhi ya leo Jumanne tarehe 23 Machi 2021, huku wengine, wakijipanga barabarani kushuhudia msafara uliobebwa ukipita.

Hadi kufikia saa 3 asubuhi, mageti yalikuwa yamefungwa kutokana na idadi kubwa ya waombolezaji waliokuwa wamejitokeza.

Kesho asubuhi Jumatano, mwili wa Dk. Magufuli, utasafirishwa kutoka Zanzibar kwenda Mwanza ambapo utaangwa na wananchi wa mkoani humo na maeneo jirani, katika Uwanja wa CCM Kirumba na baadaye, kusafirishwa kwenda Chato, mkoani Geita.

Utasafirishwa kwa barabara ukipita Misungwi- Sengerema- Geita- Buseresere- Katoro- Bwanga hadi Chato. Maeneo yote hayo inatarajiwa kushuhudia, mamia ya wananchi wakiwa wamejipanga barabarani kumuaga.

Jana Jumatatu, mwili wa Dk. Magufuli uliagwa kitaifa mkoani Dodoma ambapo marais tsa, makamu wa Rais wawili kutoka Bara la Afrika walishiriki shughuli iliyoongozwa na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.

Marais waliohudhuria ni; Uhuru Kenyatta wa Kenya ambaye pia ni mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Afrika (EAC), Filipe Nyusi wa Msumbiji, ambaye pia ni mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Felix Tshisekedi wa Congo, ambaye pia ni mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU).

Wengine ni; Lazarus Chakwera (Malawi), Azali Assoumani (Comoro), Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe, Edgar Lungu (Zambia), Mokgweetsi Masisi (Botswana) na Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini.

Pia, kulikuwa na waliowawakilisha wakuu wa nchi, wakiwemo, Makamu wa Rais Burundi, Prosper Bazombana, Makamu wa Rais Namibia, Dk. Nangolo Mbumba, Waziri Mkuu Rwanda, Edourdo Ngirente, Waziri wa Mambo ya Nje Angola, Tete Antonio, Balozi wa Uganda nchini Tanzania, Richard Kabonero.

Mwili wa Dk. Magufuli, utazikwa nyumbani kwake, Chato mkoani Geita, Ijumaa tarehe 26 Machi 2021, akiwa ameacha mjane, Janeth pamoja na watoto saba ambao ni; Suzana, Edna, Mbalu, Joseph, Jesca, Yuden na Jeremia.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online na MwanaHALISI TV kwa habari na taarifa mbalimbali

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!