Sunday , 3 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Jiji la Dodoma kugawa maeneo kwa mtandao, kisa Corona
Habari Mchanganyiko

Jiji la Dodoma kugawa maeneo kwa mtandao, kisa Corona

Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi
Spread the love

KUTOKANA na tishio la ugongwa hatari wa Coroma, halmashauri ya jiji la Dodoma limetoa utaratibu wa kuomba maeneo ya biashara kwa njia ya mtandao. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Mkurugenzi wa jiji la Dodoma, Godwin Kunambi amesena kutokana na kuwepo kwa msongamano wa waombaji wa maeneo ya biashara ofisini kwake, sasa fojunza maombi zitatolewa kwa njia ya mtandao.

Kunambi alisema maeneo yanayoombwa kuwekezwa na wafanyabiashara ni Soko la Ndugai, Standi mpya ya Mabasi na eneo la mapumziko Chinangali Park.

Alisema wakati wanaandaa utaratibu wa uchukuaji wa fomu hizo kwa njia foleni hawakutarajia kama muitikio utakuwa mkubwa lakini wananchi walijitokeza kwa wingi hali iliyosababisha wao kuamua kusitisha utaratibu huo.

Pia Kunambi alisema kuwa jiji linaendelea na uuzaji wa viwanja katika maeneo mbalimbali ikiwemo viwanja vya ujenzi wa hoteli, majengo makubwa na viwanda.

Alisema wameandaa utaratibu mpya ambao utaondoa msongamano lakini pia utamuwezesha kila mwananchi aliye popote nchini kupata fomu bila kusafiri na bila urasimu wowote.

Kunambi alisema utaratibu huo unatarajiwa kuanza rasmi April 13 mwaka huu, ambapo utakuwa ni uchukuaji wa fomu kwa njia ya mtandao, huku akiwataka wananchi kufuatilia kwenye website ya jiji la Dodoma kwa kuanzia siku hiyo.

Aidha alisema wananchi ambao tayari wameshachukua fomu April 7 mwaka huu kwa kutumia utaratibu wa awali, wataingizwa kwenye mfumo moja kwa moja na watatambulika kwa sababu tayari ni wateja wao.

Hata hivyo alisema anawasihi watanzania waondokane na dhana kuwa kuna watu maalum au wenye fedha ndio watakaofanikiwa kupata nafasi hizo za kufanyia biashara.

Alitaja maeneo ambayo viwanja hivyo vinauzwa ni Njedengwa Investment Center na tayari kuna huduma zote za kijamii na viwanja vya Ujenzi wa Viwanda katika eneo la Nala kilomita 20 kutoka mjini.

Kunambi, alivitaja viwanja vingine kuwa ni viwanja vya makazi vilivyopo katika eneo la Mtumba, Choigongwe, Kikombo na Mapinduzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

ElimuHabari Mchanganyiko

CEO NMB awataka vijana kunoa ujuzi wao

Spread the loveAfisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna, amewashauri...

Habari Mchanganyiko

TARURA kujenga madaraja 189 kwa teknolojia ya mawe

Spread the loveWakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imejipanga kujenga...

AfyaHabari Mchanganyiko

Majaliwa aipongeza GGML mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveWaziri Mkuu Kassim Majaliwa ameipongeza Kampuni ya Geita Gold Mining...

error: Content is protected !!