Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Jaji Mkuu awapa ‘mchongo’ mawakili wasio na ajira
Habari Mchanganyiko

Jaji Mkuu awapa ‘mchongo’ mawakili wasio na ajira

Spread the love

JAJI Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma, amewataka mawakili wapya na wale wa zamani ambao hawana ajira, kujikita katika masuala ya usuluhishi kwani ndiko fursa hizo zinapatikana katika nyakati hizi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Akizungumza katika hafla ya kukubali kuwapokea mawakili wapya 335, leo Ijumaa, jijini Dar es Salaam, Prof. Juma amewaeleza kuwa, wateja wengi hawaendi kupata huduma za kimahakama kwa kuwa kesi zinachukua muda mrefu, hivyo wamehamia katika masuala ya usuluhishi.

“Siku hizi wateja wengi wanapatikana katika maeneo ya usuluhishi na wengi hawaendi kupata huduma katika kesi za mahakamani sababu zinachukua muda mrefu. Taratibu za kimahakama ni nyingi sana,” amesema Prof. Juma.

Prof. Juma amesema  “kwa hiyo kwenye usuluhishi ni lazima kujikita sababu ni eneo linalokuwa na wananchi wengi hasa sekta binafsi wanapenda. Ajira imehama kutoka kuendesha mashauri mahakamani na kuhamia katika usuluhishi na majadiliano.”

Katika hatua nyingine, Prof. Juma ame Baraza la Shule ya Sheria na Shule ya Sheria kwa Vitendo, kushirikiana na vyuo vikuu katika kufanya mabadiliko ya mitaala ili ipatikane itakayosaidia wanafunzi kuajiriwa na kujiajiri katika soko la ajira la sasa.

“Hali ya nchi imebadilika sana na dunia imebadilika, sisi tunahitaji kubadilika. Kwa hiyo tunahitaji mabadiliko kwenye mitaala hasa ya shule ya sheria kwa vitendo.

Inabidi tubadilishe mitaala sio tu itawajenga katika kufanya kazi za kisheria lakini lazima iwajenge kuishi na kufanya kazi katika dunia inayotegemea teknolojia,” amesema Prof. Juma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy atangaza Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba

Spread the loveSERIKALI imesema imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha matibabu ya...

Habari Mchanganyiko

Shahidi aeleza namna Nathwani alivyomjeruhi jirani yake

Spread the loveMSIMAMIZI wa Msikiti wa Wahindi Lohana aitwae, Ankit Dawda (32)...

error: Content is protected !!