Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko BREAKING NEWS – Waziri mkuu wa zamani Japan apigwa risasi, afariki
Habari MchanganyikoTangulizi

BREAKING NEWS – Waziri mkuu wa zamani Japan apigwa risasi, afariki

Spread the love

WAZIRI Mkuu wa zamani wa Japan Shinzo Abe (67) amefariki dunia, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya kimataifa. Anaripoti Mwandishi Wetu kwa msaada wa mashirika ya habari ya kimataifa…(endelea).

Abe ambaye  anasalia kuwa waziri mkuu aliyehudumu kwa muda mrefu zaidi nchini Japan, alipigwa risasi alipokuwa akitoa hotuba ya mkutano mmoja wa kampeni.

Mshukiwa wa shambulizi hilo aliripotiwa kuwa mwanamume mwenye umri wa miaka 40 na alikamatwa  katika eneo la  tukio.

Abe alipigwa risasi mara mbili alipokuwa akitoa hotuba katika mji wa kusini wa Nara asubuhi ya  leo Ijumaa tarehe  8 Julai 2022.

Mara moja alianguka na kukimbizwa katika hospitali ya karibu. Picha zilizopigwa eneo la tukio zilimuonyesha akivuja damu.

Shirika la Kudhibiti Moto na Majanga lilithibitisha kuwa Abe alikuwa na jeraha la risasi upande wa kulia wa shingo yake, na pia alitokwa na damu chini ya ngozi chini ya sehemu ya kushoto ya kifua chake.

Haijulikani ikiwa risasi zote mbili zilimpata, au ikiwa risasi ilimpata shingoni na kutokea kwingine.

Shirika la utangazaji la taifa NHK lilisema kuwa  Abe alikuwa “na fahamu ” alipokuwa akisafirishwa hadi hospitalini, likinukuu vyanzo vya polisi.

Lakini pia ilimnukuu mwanachama mkuu wa chama cha Abe akisema hali ya kiongozi huyo wa zamani  mwenye umri wa miaka 67 ni ya “kusumbua” na kwamba alikuwa akiongezewa damu.

Aliyekuwa gavana wa Tokyo Yoichi Masuzoe alikuwa amesema hapo awali kwenye ujumbe wa Twitter kwamba  Abe alikuwa katika hali ya mshtuko wa moyo. Neno hilo mara nyingi hutumika kabla ya kifo kuthibitishwa rasmi nchini Japani.

Abe, ambaye alikuwa waziri mkuu aliyekaa muda mrefu zaidi madarakani nchini Japan, alijiuzulu mwaka 2020 akitoa sababu za kiafya. Baadaye alifichua kwamba alikuwa ameugua tena ugonjwa wa vidonda vya tumbo.

Alirithiwa na mshirika wake wa karibu Yoshihide Suga, ambaye baadaye nafasi yake ilichukuliwa na Fumio Kishida.

Matukio ya mashambulio ya bunduki ni nadra sana nchini Japani, ambapo bunduki zimepigwa marufuku – na matukio ya vurugu za kisiasa sio jambo la kawaida .

Katika mwaka 2014, kulikuwa na matukio sita tu ya vifo vya bunduki nchini Japani, ikilinganishwa na 33,599 nchini Marekani. Watu wanapaswa kufanyiwa uchunguzi mkali na vipimo vya afya ya akili ili kununua bunduki – na hata hivyo, ni aina fulani ya zinazoruhusiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua huduma maalum kwa wastaafu

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua huduma maalum kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yazindua akaunti ya Kikundi

Spread the loveBenki ya NMB imezindua akaunti ya kikundi yenye  maboresho makubwa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

error: Content is protected !!