Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Jaji avunja ukimya sakata la Mpoki kusimamishwa uwakili
Habari za Siasa

Jaji avunja ukimya sakata la Mpoki kusimamishwa uwakili

Ali and his mother - 1
Spread the love

JAJI Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma, amekitaka Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), kuwafikisha mbele ya kamati ya maadili wanachama wake watakaobainika kwenda kinyume na maadili ya taaluma hiyo, badala ya kusubiri majaji kuchukua hatua. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Prof. Ibrahim ametoa agizo hilo leo tarehe 1 Desemba 2023, baada ya kuwapokea na kuwakubali mawakili wapya 279, siku chache baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Mawakili, Jaji Ntemi Kilikamajenga, kumsimamisha uwakili kwa muda wa miezi sita, Mpale Mpoki, akituhumiwa kukiuka maadili ya taaluma hiyo.

Mpoki ambaye ni wakili mwandamizi mwenye uzoefu wa miaka 34, inadaiwa alipewa adhabu hiyo baada ya kutangaza nia ya kukata rufaa juu ya uamuzi mdogo uliotolewa na kamati hiyo, dhidi ya mteja wake, Wakili Boniface Mwabukusi, aliyeshtakiwa kwa ukiukwaji wa maadili na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).

Kiongozi huyo wa mahakama, amesema amepokea malalamiko mengi kutoka kwa baadhi ya majaji kuhusu lugha ambazo baadhi ya mawakili wanatumia mahakamani, ambazo zinaonyesha jeuri, dhihaka na dharau dhidi yao, kinyume na kanuni ya 92 ya kanuni za maadili ya mawakili.

“Naomba kukitokea tukio kama hilo isiwe jaji ndiyo alalamike, mawakili ndiyo wa kuchukua jukumu la kulalamika na kupeleka kwenye vyombo vyenu kwamba wakili mwenzetu amevunja heshima mbele ya mahakama na sisi TLS sababu tunataka kulinda taaluma yetu tunamfikisha kwenye baraza watamsikiliza baadae watatoa adhabu,” amesema Prof. Juma.

Prof. Juma amesema hata katika nchi ambazo Tanzania imeiga mifumo yake ya kisheria, ikiwemo Uingereza, mamlaka za nikinidhamu huwachukulia hatua mawakili hata kama ni waandamizi, ambao wanaonyesha dharau kwa majaji wakati wa usikilizaji kesi.

Kuhusu mawakili wapya, Prof. Juma amewataka kutowaiga mawakili wanaokiuka maadili kwenye utekelezaji wa majukumu yao, bali wawaige wale wanaozingatia maadili na kuiheshimu mahakama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!