Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Jafo awafunda wanahabari, awakumbuka utunzaji mazingira
Habari Mchanganyiko

Jafo awafunda wanahabari, awakumbuka utunzaji mazingira

Spread the love

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Seleman Jafo amewataka wanahabari nchini kujenga tabia ya upendo na kujaliana wakati wote wa shida na raha.

Pia amesema uandishi wa habari ni sehemu ya huduma ya utoaji elimu kwa jamii hivyo ni vyema wanatasnia hao wakajenga hulka ya kushirikiana kwa upendo badala ya kujengeana fitina na majungu yasiyo kuwa na sababu. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Amesema kuwa wanahabari nchini ni wadau muhimu katika kutoa elimu kwa jamii hususani elimu juu ya umuhimu wa utunzaji wa mazingira.

Jafo ametoa kauli hiyo leo tarehe 30 Julai 2022 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari wa mkoa wa Dodoma wakati wa chakula cha pamoja baada ya kumalizika kwa zoezi la kufanya usafi katika soko la Bonanza lililopo jijini Dodoma.

Jaffo amesema wanahabari wamekuwa nguzo kubwa katika kutoa elimu kwa jamii ikiwa ni pamoja kuelezea umuhimu wa utunzaji wa mazingira.

Aidha Jafo ameeleza kuwa suala la utunzaji wa mazingira ni sehemu ya ibada kwani mazingira yanaweza kufanya mabadiliko ya tabia ya nchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!