Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Meya Jacob kumng’oa Kubenea Ubungo?
Habari za SiasaTangulizi

Meya Jacob kumng’oa Kubenea Ubungo?

Spread the love

KAULI ya Boniface Jacob, Diwani wa Kata ya Ubungo (Chadema) na Meya wa Manispaa ya Ubungo, kwamba hatogombea tena udiwani katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020, inaleta taswira mpya. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Slaam…(endelea).

Kupitia ukurasa wake wa twitter leo tarehe 6 Aprili 2020, Jacob ameandika “Nimetangaza kung’atuka katika udiwani Kata ya Ubungo, muda wa madiwani utakapoisha. Sitogombea tena udiwani uchaguzi ujao..!

“Miaka 10 utumishi wangu ni kwa sababu wana-Ubungo mlinikopesha imani. Tumekuwa wote wakati wa shida na raha, mabonde na milima.”

Kwenye ujumbe wake huo, Jacob hajasema atagombea nafasi gani, lakini amekieleza chombo kimoja cha habari, kwamba anasubiri iwapo chama chake kitampa ridhaa ya kugombea ubunge katika Jimbo la Ubungo. Jimbo hilo kwa sasa linaongozwa na Saed Kubenea (Chadema).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!