Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Ireland yaahidi kuendeleza mapambano ya unyanyasaji
Habari Mchanganyiko

Ireland yaahidi kuendeleza mapambano ya unyanyasaji

Spread the love

SERIKALI ya Irelanda imeahidi kuendelea na kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto nchini ili kutokomeza vitendo hivyo vinavyo changia kurudisha nyuma shughuli za maendeleo. Anaripoti Moses Mseti, Mwanza … (endelea).

Amesema wao wataendelea kuunga jitihada za serikali za kupambana na vitendo vya ukatili na kutokomeza mimba za utotoni pamoja na ndoa za utotoni ili kuongeza kasi ya maendeleo.

Kauli hiyo aliitoa jana na Naibu Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Ireland, Adrian Fitzgerald wakati hitimisho la siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia uliofanyika katika kijiji cha Mwawile kata ya Nhundulu wilayani Misungwi mkoani Mwanza.

Fitzgerald alisema wataendelea kuunga mkono wilaya ya Misungwi katika nyanja ya afya pamoja na kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia ili kuhakikisha wanawake na watoto kukomesha vitendo hivyo.

“Tunataka familia zenye afya hapa misungwi na hatutaki kuona wanawake na wasichana wanakufa kutokana na kujifungua, tunataka kuondoa vifo vinavyotokea wakati wa kujifungua.

“Pia lazima sisi hapa tuhakikishe tunawapeleka watoto wetu wa kike shule ili tuweze kuwa na wanawake wenye uwezo wa kutunza familia zao na hiyo iende sambamba na kuondoa vipigo kwenye famili zetu,” alisema Fitzgerald.

Hata hivyo, aliwahimiza wazazi na walezi wote nchini kuhakikisha wanaacha vitendo vya kuwaozesha watoto kike ambao bado hawajafikisha umri wa miaka 18.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Kutetea Haki za Wanawake na Watoto (Kivulini) mkoani Mwanza, Yassin Ally, alisema kazi ya kupambana na vitendo vya ukatili inafanywa na makundi mengi ikiwemo jeshi la akiba (Sungusungu) katika vijiji na vitongoji vya wilaya ya Misungwi na kote nchini.

Mary Mpuya ni miongoni mwa wanawake waliofanyiwa vitendo vya ukatili na mume wake Jackson Maliki, alisema mumewe huyo kwa miaka mingi amekuwa akimfanyia vitendo vya ukatili ikiwemo kumchapa na kumfukuza nyumbani.

Alisema baada ya shirika la kivulini kufika kijijini kwao, mume wake alikwenda kusikiliza elimu iliyokuwa ikitolewa kuhusu wanaume kuacha kunyanyasa wanawake ambapo tangu siku hiyo (2018) alibadilika na kuanza kufanya shughuli za maendeleo nyumbani kwao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!