MBUNGE wa Moshi Mjini, Priscus Tarimo, ameitaka Serikali kupandisha hadhi ya utawala miji iliyokidhi vigezo, pamoja na kugawa mikoa yenye ukubwa wa kijiografia. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Akizungumza katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, leo Alhamisi, bungeni jijini Dodoma, Tarimo ameihoji Serikali kwa nini isipandishe hadhi halmashauri zilizokidhi vigezo vya kuwa jiji ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Moshi.
“Nini mpango wa Serikali kugawa au kuongeza na kupandisha hadhi maeneo ya kiutawala ambayo yamekidhi vigezo? Kugawa, kuongeza au kupandisha hadhi maeneo ya kiutawala ambayo yamekidhi vigezo? Mfano kugawa mikoa mikubwa kama Tanga na Morogoro au kupandisha hadhi halmashauri kuwa majiji kama Halmashauri ya Manispaa Moshi?” amehoji Tarimo.
Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, alimtaka Waziri Majaliwa asilijibu swali hilo akisema ni mahususi kujibiwa na mawaziri wa kisekta.
“Hili manispaa ya Moshi nadhani yenyewe liko mahususi linahitaji lijibiwe na mawaziri wa kisekta,” amesema Spika Tulia.
Leave a comment