Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Haya hapa maswali magumu ya Majaji kwa mawakili wa Ruto na IEBC
KimataifaTangulizi

Haya hapa maswali magumu ya Majaji kwa mawakili wa Ruto na IEBC

Spread the love

 

KESI ya kupinga uchaguzi wa rais mteule William Ruto katika mahakama ya Juu nchini Kenya leo Ijumaa tarehe 2 Septemba, 2022, imeingia siku yake ya nne, ambapo mawakili wa William Ruto na wale wa IEBC wakijibu maswali magumu ya majaji wa mahakama hiyo wakiongozwa na jaji mkuu Martha Koome. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Haya hapa ni baadhi ya maswali yalioulizwa na majaji hao jana jioni ambapo mawakili hao waliomba kuyajibu leo asubuhi.

Jaji Ouko kwa Wakili Mahat Somane: Kulikuwa na madai kwamba tofauti ya kura 33,000 iligunduliwa. Ni Kura ngapi zinazoshirikisha zilizopotea? Je, kuna matukio ambapo wapiga kura waliingia kwenye vituo vya kupigia kura na kuwapigia kura wagombea wa Urais pekee?

Jaji Njoki Ndungu
Njoki Ndungu kwa timu ya wanasheria wa IEBC wakiongozwa na wakili Githu Muigai

Je, nini kingetokea ikiwa mwenyekiti wa IEBC angetangaza matokeo yasiyo sahihi? Je, jukumu la makamishna wengine (IEBC) ni lipi?

Jaji Smoking Wanjala
Jaji Smokin Wanjala kwa wakili Karori: Je, jukumu la makamishna wengine wa IEBC ni lipi? Uangalizi ni nini?

Kwa Wakili Mahat: Je, mfumo wa IEBC uliingiliwa naraia wa Venezuela? Je, Raia wa Venezuela alikuwa akidumisha nini kwenye seva ya IEBC?

Je, idadi ya wapiga kura ina umuhimu gani katika kupata 50% pamoja na kura moja ya mgombea?

Je, tuchukulie kuwa kufikia wakati Bw Joseph Kinyua alipokuwa akitoa mwito wa kutaka matokeo ya uchaguzi yamuunge mkono Bw Odinga, je walijua matokeo?

Jaji Smokin Wanjala kwa timu ya wanasheria wa IEBC: Kwa nini mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati hakujumuisha matokeo ya maeneo bunge 27 kwenye kura ya mwisho ikiwa yalikuwa yamethibitishwa?

Jaji Philomena Mwilu
Jaji Philomena kwa timu ya Githu Muigai. Je, majukumu ya kikatiba ya makamishna sita wa IEBC ni yapi?

Maoni kuhusu kuondoka kwa makamishna wanne wa IEBC karibu wakati huo huo mwenyekiti (Wafula Chebukati) alikuwa karibu kutangaza matokeo. Je, kuondoka kwao kunamaanisha chochote chini ya Kifungu cha 140?

Je, kuahirishwa kwa uchaguzi wa magavana na maeneo bunge kuliathiri uchaguzi wa rais? Ikiwa waliathiriwa, kwa njia gani?

Philomena Mwilu kwa timu ya mawakili wa IEBC: Kuna mtu fulani aliwataja makamishna 4 wa IEBC kama watetezi, kwa jina lolote lile, wanasalia kuwa makamishna. Kuna hati ya kiapo kwamba wanaegemea upande mmoja. Je, kamishna anapaswa kuchukua nafasi gani? Je, wakiegemea upande mmoja, mahakama ifanye nini?

Jaji Mkuu Martha Koome
Jaji Mkuu Martha Koome kwa timu ya mawakili wa tume ya IEBC: Je, kuna tofauti kutoka kwa IEBC? Jukumu la IEBC ni kuendesha na kusimamia uchaguzi. Kwa nini mwenyekiti wa IEBC aliwagawia makamishna ‘kazi za nyumbani’ kinyume na shughuli kuu kulingana na Katiba.

CJ Koome kwa timu ya wanasheria wa IEBC: Kwa nini utiririshaji wa moja kwa moja wa matokeo ya uchaguzi wa urais ulikwama?

CJ Koome kwa wakili Mahat: Onyesha jinsi Fomu 34A katika hati za kiapo za walalamikaji zilivyobadilishwa kwa kupigwa picha.

Katika Kujibu maswali hayo jana Kiongozi wa mawakili wa IEBC Githu Muigai aliwaomba majaji hao kuwapatia muda mawakili wanaopaswa kujibu maswali kujiandaa ili kuyajibu mapema leo siku ya Ijumaa.

Hatua hiyo ilimlazimu jaji Mkuu Martha Koome kusitisha kikao hicho hadi leo Ijumaa.

1 Comment

  • Kwa maoni yangu, Odinga ameonewa katika uchaguzi huu na huyo mwenye kiti wa timu ya uchaguzi alikuwa upande moja tuu kitu ambacho ni kinyume kabisa kufuatana na majukumu ya mzimamizi wa uchaguzi, ni wazi kwamba walimuibia Odinga na kumuhifazi Ruto

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!