UBALOZI wa Marekani nchini Kenya umewataka raia wake kuchukua tahadhari kubwa nchini humo wakati huu ambapo , mahakama ya juu inatarajiwa kutoa uamuzi wake kuhusu uchaguzi wa Urais mnamo tarehe 5 Septemba 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Ubalozi huo umesema kwamba Kenya imekuwa ikikumbwa na msusuru wa ghasia kila baada ya uchaguzi.
Taarifa hiyo hususan imewataka maafisa wake waliopo katika mji wa Kisumu kuchukua tahadhari wakati ambapo uamuzi huo utakuwa ukifanywa na mahakama ya juu.
‘’Uchaguzi unaohusishwa na maandamano na mikutano mara kwa mara hutokea baada ya uchaguzi, na mara nyengine husababisha trafiki barabarani kutokana na maandamano ambayo hushirikisha ghasia hali ambayo uhitaji maafisa wa polisi kuingilia kati’’, ilisema Taarifa hiyo.
Kisumu ni mji wa eneo anakotoka mmoja wa wagombea urais Raila Odinga ambaye ameiomba mahakama kubatilisha tangazo la William Ruto kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais.
Leave a comment