Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Halima Mdee kuliburuza Bunge mahakamani
Habari za Siasa

Halima Mdee kuliburuza Bunge mahakamani

Halima Mdee, Mbunge wa Kawe
Spread the love

MBUNGE wa Kawe, Halima Mdee amesema wanatarajia kwenda mahakamani kwa ajili ya kupinga uamuzi wa Bunge wa kuwasimamisha kwa kutohudhuria vikao vya bunge kwa mwaka, anaandika Dany Tibason.

Mdee na Mbunge wa Bunda Mjini, Esther Bulaya, kwa madai ya kuwa wabunge hao wamevunja kanuni za Bunge kwa utovu wa nidhamu.
Mdee ametoa kauli hiyo leo Mjini Dodoma wakati alipokuwa akijibu baadhi ya maswali ya waandishi wa habari katika mkutano wake na waandishi juu ya matatizo makubwa yaliyopo katika bajeti ya serikali ya mwaka wa fedha 2017/18.
Amesema kuwa wameamua kufanya hivyo kwani mahakama ni muhimili ambao unatoa haki hivyo anaamini haki itatendeka.
Juni 5, mwaka huu Mbunge  wa Kawe Halima Mdee na Mbunge wa Bunda Mjini  Esther Bulaya  walisimamishwa kutohudhuria vikao vyote vya bunge linaloendelea mpaka mkutano ujao wa Bunge la Bajeti la mwaka 2018/19 ambapo hukumu hiyo iliungwa mkono na wabunge wengi wa CCM kutokana na hoja ya mbunge wa Viti Maalum, Juliana Shonza.

1 Comment

  • Tunakutakia kila la kheri! Hata hivyo tunashukuru kwamba bunge halioneshwi mbashara kwani vituko vyenu vinatia aibu! Acha tuwe tunawasikiliza tu kwenye redio!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!