Monday , 5 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Halima Mdee kuliburuza Bunge mahakamani
Habari za Siasa

Halima Mdee kuliburuza Bunge mahakamani

Halima Mdee, Mbunge wa Kawe
Spread the love

MBUNGE wa Kawe, Halima Mdee amesema wanatarajia kwenda mahakamani kwa ajili ya kupinga uamuzi wa Bunge wa kuwasimamisha kwa kutohudhuria vikao vya bunge kwa mwaka, anaandika Dany Tibason.

Mdee na Mbunge wa Bunda Mjini, Esther Bulaya, kwa madai ya kuwa wabunge hao wamevunja kanuni za Bunge kwa utovu wa nidhamu.
Mdee ametoa kauli hiyo leo Mjini Dodoma wakati alipokuwa akijibu baadhi ya maswali ya waandishi wa habari katika mkutano wake na waandishi juu ya matatizo makubwa yaliyopo katika bajeti ya serikali ya mwaka wa fedha 2017/18.
Amesema kuwa wameamua kufanya hivyo kwani mahakama ni muhimili ambao unatoa haki hivyo anaamini haki itatendeka.
Juni 5, mwaka huu Mbunge  wa Kawe Halima Mdee na Mbunge wa Bunda Mjini  Esther Bulaya  walisimamishwa kutohudhuria vikao vyote vya bunge linaloendelea mpaka mkutano ujao wa Bunge la Bajeti la mwaka 2018/19 ambapo hukumu hiyo iliungwa mkono na wabunge wengi wa CCM kutokana na hoja ya mbunge wa Viti Maalum, Juliana Shonza.

1 Comment

  • Tunakutakia kila la kheri! Hata hivyo tunashukuru kwamba bunge halioneshwi mbashara kwani vituko vyenu vinatia aibu! Acha tuwe tunawasikiliza tu kwenye redio!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!